Msanii wa mziki wa Kizazi kipya nchini Tanzania, Hamis Mwinjuma @mwanaFA ameweka rekodi ya kufika Kilele cha Uhuru cha mlima Kilimanjaro. Msanii @MwanaFA ni miongoni mwa wasanii walioshiriki kampeni iliyoandaliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, @HKigwangalla ya #TwenzeZetuKileleni.
Msanii wa mziki wa Kizazi kipya nchini Tanzania, Hamis Mwinjuma - MwanaFA akiwa juu ya kilele cha Afrika (Mlima Kilimanjaro) akiwa ameshika picha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli ili kuiambia dunia kwamba Tanzania imeamua kujenga uchumi imara na madhubuti kwa Uzalendo wa hali ya juu, Uadilifu, Muaminifu na Kuchapa Kazi.
Toa Maoni Yako:
0 comments: