TRENDING NOW





 Na Mwandishi Wetu.

 Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imekutana na kufanya mazungumzo na watangazaji na waandaaji wa kipindi cha Good Morning kinachorushwa na Wasafi FM, ambapo imewakumbusha umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya uandishi wa habari katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Kikao hicho kimefanyika leo, Septemba 2, 2026, katika Makao Makuu ya JAB, Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam, kikilenga kuimarisha uelewa wa watangazaji hao kuhusu misingi ya weledi, uwajibikaji na matumizi sahihi ya majukwaa ya habari.

Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, amefafanua matakwa ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229; Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Sura ya 306; pamoja na kanuni zake zinazopaswa kuzingatiwa katika utayarishaji na utangazaji wa maudhui.

Wakili Kipangula ameeleza kuwa kuzingatia sheria na maadili ni msingi wa kulinda heshima ya taaluma, haki za watu wanaohusika katika maudhui na imani ya jamii kwa Waandishi wa Habari.
Baada ya mazungumzo hayo, watangazaji wakongwe Gelard Hando na Hilary Mtuta, maarufu kama Zembwela, walikabidhiwa vitambulisho vyao vya ithibati ya uandishi wa habari baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari.

Makabidhiano hayo yamekamilisha hatua ya kuwatambulisha rasmi kama Waandishi wa Habari wenye ithibati, wenye wajibu wa kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, maadili na uwajibikaji.


Kutoka kushoto: Tahir Mussa, Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade; Juma Burhan, Mkurugenzi Mtendaji wa ZEEA; na Fatma Ahmed, Mkuu wa Huduma za Kibenki kwa Wafanyabiashara, Benki ya Stanbic, katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Zanzibar jana kutangaza ushirikiano huo.
Stanbic Bank Tanzania imetangaza udhamini wa TZS milioni 200 kwa maonesho ya Fahari ya Zanzibar 2026, hatua inayoonesha dhamira yake ya kuendelea kuchangia ukuaji wa uchumi wa Zanzibar na kuwawezesha wafanyabiashara, wajasiriamali na jamii kwa ujumla.
 
Maonesho hayo yatafanyika kuanzia tarehe 4 hadi 14 Septemba 2026 katika Viwanja vya Maisara, Zanzibar, yakibeba kaulimbiu “Bidhaa Zetu Ndio Fahari Yetu.” Zaidi ya washiriki 300 na wageni 15,000 wanatarajiwa kushiriki katika tukio hilo, linalolenga kuhamasisha matumizi ya bidhaa zinazozalishwa nchini. Maonesho hayo yameandaliwa na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE).
 
Kama mdhamini mkuu, Stanbic Bank itatumia maonesho hayo kuonesha suluhisho mbalimbali za kifedha zinazolenga kusaidia ukuaji wa biashara, kuwezesha biashara za ndani na za kimataifa, pamoja na kukuza ushiriki wa wafanyabiashara katika fursa za masoko mapya.
 
Akizungumza kuhusu ushiriki wa benki hiyo, Fatma Ahmed, Mkuu wa Huduma za Kibenki kwa Wafanyabiashara, Stanbic Bank Tanzania, alisema ushirikiano huo unaakisi imani ya benki katika nafasi ya Zanzibar kama kitovu muhimu cha biashara na uwekezaji.
 
"Fahari ya Zanzibar ni jukwaa linaloonesha ubunifu, juhudi na uwezo wa wafanyabiashara wa Zanzibar. Sisi tunaendelea kujenga mazingira yatakayowasaidia kukuza biashara zao, kuongeza ushindani na kufikia masoko mapana zaidi. Zanzibar ni nyumbani kwetu, na tutaendelea kuunga mkono safari yake ya maendeleo ya kiuchumi," alisema.
 
Maonesho hayo pia yatahusisha mijadala na shughuli mbalimbali zinazolenga vijana, ubunifu, utalii, sanaa, biashara na ujumuishaji wa kiuchumi.

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akizindua Programu ya Mining for a Brighter Tomorrow (MBT) katika eneo la Nyamongo, mkoani Mara, inayolenga kupanua fursa za maeneo ya uchimbaji, taarifa za kijiolojia na leseni kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Helikopta ikifanya utafiti wa madini kwa njia ya anga katika eneo la Nyamongo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya MBT, hatua itakayosaidia kupata taarifa za kijiolojia kwa ajili ya utafiti wa kina na uchorongaji katika maeneo yaliyotengwa kwa wachimbaji wadogo.


Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha Ndugu Richard Marcellino Kayombo kuwa Katibu Tawala, Mkoa wa Pwani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.
Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha CP Salum Rashid Hamduni kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha Mhe.
Stanslaus Haroon Nyongo kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.


Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimuapisha Mhe.Alexander Pastory Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Viongozi wakila kiapo cha Maadili kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02
Septemba, 2026.

Viongozi pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya Uapisho wa Wakuu wa mikoa ya Mbeya, Geita, Pwani, Mwanza pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akizungumza na Viongozi baada ya kuwaapisha Wakuu wa mikoa ya Mbeya, Geita, Pwani, Mwanza pamoja na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kwenye picha na Wakuu wa Mikoa baada ya hafla ya Uapisho wa Viongozi mbalimbali iliyofanyika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar tarehe 02 Septemba, 2026.

Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Yvonne Maruma akizungumza katika Wiki ya Ubunifu Tanzania 2026 ambapo alizungumzia namna ya Vodacom inavyounganisha Watanzania na kuleta tija kupitia Zaidi ya Mtandao: Hususani Watengeneza maudhui na Majukwaa Mtandaoni kwa kuwapa mtandao bora na simu janja zinazo unga mkono ubunifu wao.

Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Yvonn Maruma (kulia) akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango Dr. Blandina Kilama baada ya kumaliza majadiliano ya namna ya kuziunganisha sauti za Watanzania: Watengeneza maudhui na Majukwaa Mtandaoni. Tukio hilo limefanyika katika Wiki ya Ubunifu Tanzania leo hii.
Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Yvonne Maruma (kulia) akisalimiana na Mhariri Mtendaji mkuu wa kampuni ya Mwananchi Communications Limited baada ya kumaliza majadiliano ya namna ya kuziunganisha sauti za Watanzania: Watengeneza maudhui na Majukwaa Mtandaoni. Tukio hilo lilifanyika katika Wiki ya Ubunifu Tanzania leo hii.
Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Yvonne Maruma (wa pili kushoto), akisikiliza majadiliano yaliyohusu namna ya kuziunganisha sauti za Watanzania: Watengeneza maudhui na Majukwaa Mtandaoni. Tukio hilo lilifanyika wakatib wa Wiki ya Ubunifu Tanzania.
Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Yvonne Maruma (kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communications Limited Rosalynn Mndolwa-Mworia (wa pili wa kushoto), Meneja wa Uchunguzi wa Vodacom Tanzania Joseph Mnyune (kushoto) na Meneja Biashara Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communication Limited Tess Aloyce (wa pili kulia) wakizungumza wakati wa Wiki ya Ubunifu Tanzania ambapo Vodacom Tanzania walishiriki katika majadiliano ya namna ya kuziunganisha sauti za Watanzania: Watengeneza maudhui na Majukwaa Mtandaoni. Tukio hilo lilifanyika katika Wiki ya Ubunifu Tanzania leo hii.

Na Mwandishi Wetu.

Ni katika Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026

Katika Wiki ya Ubunifu Tanzania (IWTz) 2026, Vodacom Tanzania imeonyesha mchango wa mtandao, ubunifu na ujasiriamali katika kufanikisha Dira ya Maendeleo Tanzania 2050. Tukio hilo limewakutanisha wabunifu, wajasiriamali, watunga sera, wawekezaji, vijana na wadau mbalimbali chini ya kauli mbiu: “Kutoka Matarajio hadi Mageuzi: Kuibua Njia ya Tanzania Kuelekea Ustawi Jumuishi.”

Vodacom imeshiriki katika mjadala kuhusu uchumi wa watengeneza maudhui, maonesho, mikutano na wadau na shughuli za kuelimisha kuhusu usalama wa mtandao.

Akizungumza katika mjadala wa watengeneza maudhui na majukwaa mtandaoni, Mkuu wa Idara ya Chapa na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Yvonne Maruma, alisema mtandao una thamani zaidi kupitia fursa unazowawezesha Watanzania kuzipata katika elimu, biashara na ubunifu.

Kupitia Vodacom Youth Base (VYB), kampuni inaendelea kuwawezesha watengeneza maudhui kubaki mtandaoni na kukuza shughuli zao za kidijitali. Ushiriki wa Vodacom katika IWTz 2026 unaunga mkono malengo ya Dira ya Maendeleo 2050 kupitia mageuzi ya kidijitali, uvumbuzi na ukuaji wa uchumi jumuishi.