TRENDING NOW






Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Meneja wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Zanzibar, Bi. Mariam Saleh Tuzo ya shukran kutokana na mchango wa Mfuko huo kuwa miongoni mwa Taasisi zilizofanikisha kufanyika kwa Kongamano hilo ambalo ni sehemu ya Tamasha la 10 la Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar usiku wa kuamkia leo Agosti 12, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Taasisi zilizopatiwa tuzo
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Kushoto) na mkewe Mama Mariam Mwinyi (mwenye raba nyekundu), wakitembelea mabanda ya Maonesho baada ya kuzindua Tamasha la Kizimkazi Agosti 12, 2026

Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, akiwa na Tuzo ya shukrani baada ya kukabidhiwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kukabidhiwa.

Zanzibar, Agosti 12, 2026

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameutunuku Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) tuzo ya kutambua mchango wake katika kuwezesha kufanyika kwa Mdahalo wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, uliofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, usiku wa kuamkia leo, Agosti 12, 2026.

Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Meneja wa PSSSF Zanzibar, Bi. Mariam Saleh, kwa niaba ya Mfuko, ikiwa ni sehemu ya utambuzi kwa taasisi na wadau walioshiriki katika kuwezesha mdahalo huo, uliofuatiwa na Maonesho ya Picha za Tamasha la Kizimkazi.

Mdahalo huo umefanyika sambamba na Tamasha la 10 la Kizimkazi (Kizimkazi Festival 2026), linalofanyika Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ambapo tamasha hilo limeanza rasmi leo kwa matembezi pamoja na uzinduzi uliofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Ushiriki wa PSSSF katika mdahalo huo unaakisi dhamira ya Mfuko ya kushirikiana na Serikali, taasisi na wadau mbalimbali katika kuunga mkono mijadala yenye umuhimu kwa jamii, mazingira na maendeleo endelevu.

Aidha, PSSSF inawakaribisha wanachama na wananchi kutembelea banda la Mfuko katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi yanayoanza leo, Agosti 12, 2026, kwa ajili ya kupata elimu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Mfuko, amesema Afisa Uhusiano Mkuu wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady.

 




Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wanachama wa Chama hicho katika Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.

Shamra shamra za Mapokezi ya Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, baada ya kuwasili Maskani Kaka Kisonge, Michenzani Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026.




Na Mwandishi wetu- Kibaha, Pwani.

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kupitia idara ya afya imetoa mafunzo kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii na kufanya tathmini ya magonjwa yasiyoambukiza na namna ya kukabiliana nao.

Mafunzo hayo yametolewa na Wizara ya Afya kupitia taasisi ya TANCDA inayojihusisha na utoaji wa elimu kwa umma juu ya magonjwa yasiyoambukiza na namna ya kupambana nayo ikiwemo kubadilisha mtindo wa maisha.

Mratibu kitengo cha magonjwa yasiyoambukiza kutoka Wizara ya Afya Dkt Grace Gembe amesema magonjwa yasiyoambukiza yamekuwa kwa kasi sana ni muhimu sana wananchi waweze kupata uelewa na elimu ili kujilinda.
Gembe amesema, anaamini mafunzo haya yatakuwa na tija kwa wahudumu hawa wa ngazi ya jamii ambapo watakaporudi kwenye mitaa yao watakuwa walimu wazuri kwenye kuelemisha jamii.

Kwa upande wa Mganga Mkuu Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dkt Catherine Saguti amesema kwa siku ya leo wametoa mafunzo kwa vijana 40 ila wanajumla ya vijana 135 katika mitaa yote 73 ya Manispaa ya Kibaha.
Amesema, vijana hao wote watapata mafunzo ya namna ya kutoa elimu kwa jamii juu ya magonjwa yasiyo yakuambukiza katoka ngazi ya jamii na namna ya kukabiliana nayo.

Baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo, vijana hao wamepatiwa kitabu kinachoelezea magonjwa mbalimbali yasiyoambukiza na namna ya kujitambua pindi unapokuwa na dalili zilizoanishwa humo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali Mama Fatma Karume, Mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, ambaye anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Lumumba, Zanzibar, tarehe 11 Agosti, 2026
Na Janeth Raphael - MichuziTv

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka wananchi wanaomiliki silaha kuhakikisha wanakamilisha taratibu zote za kisheria na vibali vinavyohitajika kabla ya Agosti 30, 2026, akieleza kuwa operesheni maalum ya ukaguzi wa silaha itaanza mara baada ya muda huo.

Chalamila ametoa agizo hilo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo , akisisitiza kuwa wamiliki ambao kwa sababu mbalimbali, ikiwemo kusahau au kutokuwa na uelewa wa kutosha kuhusu taratibu, hawajakamilisha malipo ya vibali au hatua nyingine za kisheria, wanapaswa kutumia muda uliopo kufika katika mamlaka husika na kurekebisha hali hiyo.

Amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha silaha zinazomilikiwa na wananchi katika Mkoa wa Dar es Salaam zinakuwa na kumbukumbu na vibali halali vinavyotambulika kisheria, kabla ya kuanza kwa operesheni hiyo.

Kwa upande mwingine, Mkuu huyo wa Mkoa amewataka watu wanaomiliki silaha bila kufuata sheria kuzisalimisha kwa hiari katika Jeshi la Polisi au kituo cha Polisi kilicho karibu kabla ya operesheni kuanza. Amesisitiza kuwa hatua hiyo inaweza kusaidia wahusika kuepuka kukumbana na hatua za kisheria zitakazochukuliwa baada ya ukaguzi kuanza.

Aidha, Chalamila ametoa mwito kwa familia ambazo ndugu zao wamefariki huku wakiacha silaha zenye vibali halali kuhakikisha hazizifichi wala kuzihamisha bila kufuata utaratibu. Badala yake, amewataka kuwasilisha taarifa pamoja na silaha hizo kwa mamlaka husika ili kupata maelekezo ya kisheria kuhusu namna ya kushughulikia umiliki huo.

Kuhusu silaha zinazoripotiwa kuibiwa, amewataka wamiliki kutoa taarifa Polisi na kufuata taratibu zote zinazohitajika. Amesisitiza kuwa silaha hizo zinapopatikana, wahusika hawapaswi kuzificha au kuendelea kuzitumia bila kufuata maelekezo ya mamlaka.

Chalamila amesisitiza kuwa Agosti 30, 2026 ndiyo mwisho wa muda uliotolewa kwa wamiliki kuhakikisha wanakamilisha taratibu zao, akieleza kuwa baada ya tarehe hiyo operesheni maalum ya ukaguzi itaanza na yeyote atakayebainika kumiliki silaha kinyume cha sheria atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.

Amewataka wananchi kutotumia muda uliobaki kupuuza agizo hilo, bali kuhakikisha mapema kuwa umiliki wa silaha zao uko katika hali halali na unaotambulika na mamlaka, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha udhibiti na usalama wa silaha katika Mkoa wa Dar es Salaam.
EY Tanzania imezindua kwa mafanikio Ripoti ya Sekta Ndogo ya Benki Tanzania 2025, tukio lililowakutanisha viongozi wa sekta ya fedha, wadhibiti na wataalamu wa benki kujadili mwelekeo wa sekta hiyo katika mazingira yanayobadilika kwa kasi. Mada kuu ya mwaka huu ilikuwa“Akili Mnemba katika Sekta ya Benki: Faida ya Ushindani Ijayo”, ikilenga kuonesha jinsi Akili Mnemba (AI) inavyobadilisha ushindani katika huduma za kifedha.
Majadiliano hayo yaliongozwa na Bi. Irene Morris (EY) ambapo aligusia safari ya mageuzi ya sekta ya benki kutoka mifumo ya jadi inayotegemea mahusiano ya karibu na wateja (relationship banking) hadi benki za kidijitali, majukwaa ya kifedha (platform banking) na mifumo ya ikolojia ya huduma za kifedha (ecosystem banking). Washiriki walijadili namna AI, data na teknolojia vinavyoboresha uzoefu wa wateja, kuimarisha usimamizi wa hatari, kuongeza ufanisi wa shughuli za benki na kuibua fursa mpya za ukuaji wa biashara.

Tukio hilo pia liliangazia mwenendo muhimu unaoendelea kuunda sekta ya benki nchini Tanzania, ikiwemo ukuaji endelevu wa sekta, kuongezeka kwa ujumuishaji wa kifedha, matumizi yanayoongezeka ya huduma za kifedha za kidijitali, pamoja na umuhimu wa ubunifu katika kujenga taasisi za kifedha zilizo imara na zenye uwezo wa kukabiliana na mahitaji ya siku zijazo.
Aidha, washiriki walipata fursa ya kujadili kiwango kipya cha utoaji taarifa za kifedha (IFRS 18) na athari zake kwa sekta ya benki. Majadiliano yalioongozwa na Bw. Joshua Luoga (EY) ambapo alitoa ufahamu kuhusu mabadiliko yajayo katika uwasilishaji wa taarifa za kifedha, upimaji wa utendaji wa kifedha pamoja na kuongeza uwazi kwa wadau wa sekta ya fedha.
EY Tanzania inawashukuru kwa dhati wazungumzaji, (Bw. Rweyemamu Barongo, Kiongozi wa Kitengo cha Ubunifu wa Akili Mnemba (AI) na Data katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Tobias Swai, Mhadhiri Mwandamizi na Mkuu wa Idara ya Fedha katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Pamoja na Bw. Robert Bwana, Mwanasayansi Mwandamizi wa Data katika Benki ya NMB) washiriki na wadau wote waliochangia mjadala wenye tija kuhusu mustakabali wa sekta ya benki nchini Tanzania na nafasi ya teknolojia na ubunifu katika kuendeleza ukuaji wa sekta hiyo.


Na Mwandishi Wetu.

JAMII ya Wandondi na Wandwewe, imetoa mwito wa kitaifa na kimataifa kwa watu wote wenye nia njema kuungana katika Dua Maalum kwa ajili ya Amani, Umoja, Maridhiano, Mshikamano na Ulinzi wa Maisha ya Binadamu.

Dua hiyo ni mwito wa pamoja unaolenga kuwakutanisha watu wa imani, mila, tamaduni na mitazamo mbalimbali katika kusimama kwa pamoja kutetea amani, utu, uhai, mshikamano na heshima kwa mwanadamu, bila kujali tofauti za dini, kabila, rangi, taifa, utamaduni, itikadi au hali ya kijamii.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Chifu Felix G. L. Mfunda, kwa niaba ya jamii ya Wandondi na Wandwewe amesema dua hiyo itafanyika  Agosti 12, 2026,  ambapo Misa Maalumu ya Kikatoliki itafanyika katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Mhangazi, Parokia ya Kitanda, Namtumbo, Ruvuma. huku akitoa  mwito wa amani na maridhiano.

Aidha, kuanzia jioni ya Agosti 13 hadi mchana wa Agosti 14, 2026, kutafanyika dua, na shughuli za jadi zitakazoambatana na ngoma na sanaa mbalimbali za asili za Wandwele na Wandondi.

Jamii mbalimbali za Mkoa wa Ruvuma, zikiwemo Makumbo, Lizombe na Makiwa, zinatarajiwa kushiriki katika shughuli hizo zinazolenga kuenzi urithi wa tamaduni, kuimarisha undugu na mshikamano, pamoja na kukuza amani kati ya jamii.

Mfululizo huo utakamilishwa Agosti 16, 2026, kwa Dua Maalumu ya Kiislamu itakayofanyika jioni kwa ajili ya kuiombea Tanzania, Afrika na dunia nzima.
Ambapo  amesema Dunia ya leo inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo migogoro, vita, chuki, migawanyiko ya kijamii, changamoto za kiuchumi, ukosefu wa usawa na athari za mabadiliko ya tabianchi.

“Katika mazingira haya, tunapaswa kutambua kwamba amani si wajibu wa Serikali pekee; ni wajibu wa kila mwanadamu.Tunatoa mwito kwa viongozi wa kitaifa na kimataifa, viongozi wa dini, viongozi wa kimila, wasomi, vijana, wanawake, mashirika ya kiraia na wananchi wote kutumia nafasi zao kujenga madaraja ya maelewano badala ya kuta za migawanyiko.

“Tunasisitiza umuhimu wa mazungumzo, kusikilizana, kusameheana, kuheshimiana na kutafuta suluhu za amani katika kila tofauti inayojitokeza.”

Aidha amesema ulinzi wa maisha ni wajibu wa pamoja akifafanua maisha ya mwanadamu ni tunu kubwa na hayapaswi kuwekwa rehani kwa sababu ya tofauti za kisiasa, kidini, kikabila, kiuchumi, kijamii au kiitikadi.

Ameongeza kwa msingi huo, wanatoa mwito wa kuheshimiwa kwa utu wa binadamu, haki ya kuishi, usalama wa raia na ulinzi wa watoto, wanawake, wazee na makundi yote yaliyo katika mazingira hatarishi.

“Tunasisitiza tofauti zetu zisigeuke kuwa sababu ya kupoteza maisha ya watu.Kila jamii ina wajibu wa kulinda maisha na kujenga mazingira ambayo kila mwanadamu anaweza kuishi kwa usalama.

Pia amesema kuhusu amani, afya na ulinzi wa mazingira ni kwamba amani ya kweli haiwezi kutenganishwa na afya ya jamii, usalama wa chakula, maji safi, mazingira salama na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

“Uharibifu wa mazingira, ukataji wa misitu, uharibifu wa vyanzo vya maji, upotevu wa bayoanuai na athari za mabadiliko ya tabianchi vinaweza kuongeza changamoto za kijamii na kiuchumi na kuhatarisha maisha ya watu.

“Kwa hiyo, tunatoa mwito wa kuunganisha juhudi za amani, afya, mazingira na maendeleo endelevu kwa ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Akieleza zaidi amesema katika dua kwa Watanzania ,Afrika na Dunia amefafanua Tanzania iendelee kuwa taifa la amani, umoja, mshikamano na utulivu na kwa Afrika ipate amani na utulivu wa kudumu.

Pia migogoro na vita duniani zipungue na hatimaye kumalizika na kuongeza viongozi wapate hekima, busara, uadilifu na moyo wa kuhudumia watu.Vijana wapate fursa za elimu, ajira, ubunifu, ujasiriamali na maendeleo.

Kwa watoto walindwe dhidi ya ukatili, unyanyasaji na mazingira yanayohatarisha maisha yao. Wanawake, wazee na makundi yaliyo katika mazingira magumu walindwe na kuheshimiwa.Wagonjwa na wote wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali wapate faraja, matumaini na huduma stahiki na mazingira.

Kuhusu ujumbe kwa Watanzania amesema wanawakumbusha Umoja wetu ni nguvu yetu, amani yetu ni utajiri wetu, na maisha ya kila Mtanzania ni sehemu ya thamani ya Taifa letu.

“Tunapaswa kukataa chuki, uchochezi, ubaguzi, vurugu na lugha zinazogawa jamii. Badala yake, tujenge utamaduni wa kusikilizana, kuheshimiana, kusameheana, kusaidiana na kutatua tofauti zetu kwa njia za amani.

“Tanzania yenye amani na mshikamano ni msingi muhimu wa maendeleo ya watu wake na mchango mkubwa kwa amani ya Afrika na dunia.”


Dar es Salaam, Tanzania: Afrika inapaswa kutumia zaidi mitaji yake ya ndani, kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kukuza masoko ya fedha ya ndani ili kuziba pengo la ufadhili wa miundombinu na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu, Benki ya Stanbic Tanzania imesema.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wanahisa wa Africa50 na Jukwaa la Miundombinu la Afrika (Africa Infrastructure Forum), lililofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam, likiwakutanisha viongozi wa kisiasa, wataalamu wa masuala ya fedha na maendeleo kujadili namna taasisi za Afrika zinavyoweza kushirikiana kufadhili maendeleo ya bara, wakati ambapo uwekezaji wa kimataifa unazidi kuwa wa kuchagua.

Akizungumza katika kikao cha mjadala kilichokuwa na mada “Pace Setters: African-Designed, African-Led” (Waongoza Njia: Yaliyobuniwa na Kuongozwa na Waafrika), Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania, Manzi Rwegasira, alisema Afrika tayari ina taasisi imara za kifedha, lakini kinachohitajika sasa ni kuongeza uwezo wa taasisi hizo ili kukidhi mahitaji makubwa na yanayoongezeka ya miundombinu barani.

“Majibu yote mazuri yatatolewa, lakini nadhani yote yanaishia kwenye suala la ukubwa. Tunahitaji kufikiria namna ya kuongeza kiwango cha kile ambacho tayari tunacho katika bara hili,” alisema Rwegasira.

Akielezea mchango wa taasisi kama Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Africa50, Rwegasira alisema taasisi hizo pekee haziwezi kugharamia mahitaji yote ya miundombinu ya Afrika.

Alisema Afrika inapaswa kuongeza uhamasishaji wa rasilimali za ndani, hususan kupitia masoko imara na yenye kina zaidi ya mitaji ya ndani, ambayo yanaweza kusaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya uwekezaji wa muda mrefu.
“Tunapaswa kutumia vizuri zaidi masoko yetu ya ndani ya hati fungani za serikali. Bado ni madogo na hayana kina cha kutosha. Tunahitaji kuyakuza,” alisema.

Rwegasira pia alitaja ushirikiano wa kikanda kuwa nguzo muhimu katika kufungua vyanzo vikubwa zaidi vya mitaji, akisema nchi za Afrika zinapaswa kuacha kufanya kazi kwa kujitenga na badala yake kutumia nguvu ya pamoja ya rasilimali zilizopo barani.

“Labda ushirikiano wa kikanda ndio mahali tunapoweza kuanzia. Tunahitaji kufanya kazi pamoja kwa ushirikiano ili kutumia mitaji tuliyonayo,” alisema.

Aliongeza kuwa mifumo bunifu ya ufadhili, ikiwemo sekuritizasheni (securitisation) na urejelezaji wa mali za miundombinu (infrastructure asset recycling), inaweza kusaidia serikali kupata uwekezaji wa ziada bila kutegemea pekee vyanzo vipya vya mitaji.

“Securitisation inakuruhusu kutumia tena mtaji uleule tulionao. Ikiwa tunaweza kurejeleza mali za miundombinu, tunaweza kutumia kile ambacho tayari kimejengwa kufadhili miundombinu mipya,” alisema.

Mijadala hiyo iliakisi lengo pana la jukwaa hilo la kuendeleza mfumo wa ufadhili unaoongozwa na Waafrika kupitia **New African Financial Architecture for Development (NAFAD)**, unaolenga kuunganisha nguvu za benki za Afrika, wawekezaji wa kitaasisi, kampuni za bima, taasisi za fedha za maendeleo na serikali katika kufadhili miradi ya miundombinu kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza kando ya mkutano huo, Mkuu wa Kitengo cha Corporate and Investment Banking wa Stanbic Bank Tanzania, Ester Manase, alisema jukwaa hilo limeonesha kuwa ushirikiano ni msingi muhimu katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu barani Afrika.
“Mkutano huu umekuwa na manufaa makubwa kwetu kama benki kwa sababu umewakutanisha wadau muhimu ambao wamejikita katika kusaidia maendeleo ya miundombinu barani Afrika,” alisema Manase.

Alisema miundombinu ni kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi kwa kuwa hurahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo na bidhaa nyingine, kuwezesha biashara ya kimataifa na kuchangia katika maendeleo ya uchumi kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Manase, somo kubwa zaidi kutoka katika mkutano huo wa siku mbili ni umuhimu wa ushirikiano kati ya benki za biashara, taasisi za fedha za maendeleo, kampuni za bima, serikali na wawekezaji binafsi, kwa kuwa hakuna taasisi moja inayoweza kugharamia mahitaji ya muda mrefu ya miundombinu ya Afrika pekee.

“Jambo kubwa nililojifunza ni umuhimu wa ushirikiano. Kila mdau ana nafasi muhimu ya kutekeleza, lakini hakuna mmoja wetu anayeweza kufikia malengo haya peke yake,” alisema.

Manase alieleza kuwa ingawa benki za biashara zina nafasi muhimu katika ufadhili wa miundombinu, miradi hiyo inahitaji mitaji ya muda mrefu na yenye uvumilivu, ambayo inaweza kupatikana kupitia ushirikiano na taasisi za fedha za maendeleo pamoja na wawekezaji wa kitaasisi.

“Benki za biashara zinaweza kusaidia ufadhili wa miundombinu kwa kiwango fulani. Kwa kuwa hii ni uwekezaji wa muda mrefu, tunahitaji taasisi za fedha za maendeleo, kampuni za bima, pamoja na sekta ya umma na binafsi kufanya kazi kwa pamoja,” alisema.

Mtendaji huyo pia alisema Tanzania iko katika nafasi nzuri kimkakati ya kuwa lango kuu la usafirishaji na biashara kwa Afrika Mashariki, akitaja uwekezaji unaoendelea katika bandari, reli ya Standard Gauge Railway (SGR) na miundombinu ya barabara.

“Tanzania iko katika eneo la kimkakati sana. Tuna nchi jirani nane, ambapo sita kati ya hizo hazina bandari. Hii inatupa fursa ya kipekee ya kuwa kitovu cha ukanda huu,” alisema.

Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, alisema ufadhili wa miundombinu unapaswa hatimaye kuboresha maisha ya wananchi na hivyo kwenda sambamba na uwekezaji katika rasilimali watu.

Dkt. Kikwete alisema ongezeko la idadi ya vijana barani Afrika linaweza kuwa faida kubwa zaidi ya kiuchumi kwa bara hilo ikiwa serikali zitawekeza katika elimu bora, ukuzaji wa ujuzi na fursa za ajira.

Alisisitiza kuwa barabara, reli na miradi ya nishati haipaswi kuonekana kama mafanikio ya maendeleo yenyewe, bali kama nyenzo za kuongeza uzalishaji, kukuza biashara na kufikia ustawi wa pamoja.

Dar es Salaam-Tanzania, 07th August, 2026: As the International Beer Day is being marked today, Serengeti Breweries Limited (SBL) is marking it uniquely demonstrating the world-class quality of its products. This follows the receiving of Gold Quality Awards – 2026 from the internationally renowned Monde Selection for three of Serengeti Breweries’ brands: Serengeti Lite, Serengeti Lager and Serengeti Lemon.

The Gold Quality Awards, by the Monde Selection, are presented to products that meet the highest international quality standards following a rigorous evaluation by an independent panel of international experts. Products are assessed against a range of criteria, including overall quality, taste, appearance, innovation, consumer information and user experience, to ensure they meet globally recognised benchmarks of excellence.

Founded in 1961 in Brussels, Belgium, Monde Selection is an independent international quality institute specialising in the evaluation of consumer products. For more than 65 years, the institute has assessed thousands of products across various categories, including food, beer, spirits, health and dietary products, and cosmetics. Each year, evaluations are conducted by more than 80 international experts, with products from approximately 150 countries having been submitted for assessment over the years.

This recognition reflects Serengeti Breweries Limited's continued commitment to producing world-class beverages through sustained investment in advanced brewing technologies, robust quality assurance systems and innovation that places consumers at the heart of everything the company does.

Commenting on the achievement, Joseph Cheloti, Supply Chain Director at Serengeti Breweries Limited, said the awards are a testament to the company's unwavering commitment to quality across its product portfolio.

"Receiving the Gold Quality Awards from Monde Selection is a tremendous honour and a strong endorsement that our products meet internationally recognised quality standards. We are proud of this achievement, which reflects the dedication of our people, the quality of the ingredients we use, and the strength of our production processes. Above all, we thank our consumers for their continued trust and loyalty."

He added that the company will continue investing in quality, innovation and product development to ensure consumers in Tanzania and beyond continue to enjoy beverages that meet the highest international standards.

The company’s renowned Spirits Brand, TZEE, also won the Gold Quality Award – 2026. Winning four Gold Quality Awards simultaneously further strengthens Serengeti Breweries Limited's position among leading beverage manufacturers committed to delivering internationally recognised quality while proudly showcasing Tanzania's excellence on the global stage.