TRENDING NOW





DODOMA, TANZANIA — September 8, 2026.

Day One of the Bootcamp at Msalato Girls Secondary School in Dodoma began with the girls taking an active role in the learning process.

Working in groups, the students engaged in discussions, sharing ideas and exploring different challenges that could be addressed through technology.

The discussions gave the girls an opportunity to work together, listen to different perspectives and develop ideas as a team.

After the group discussions, the students came together for presentations.

Standing before the whole class, the groups presented the ideas they had developed during their discussions, giving each student an opportunity to participate and share what her group had explored.

Through this process, the girls were beginning to build important skills in teamwork, communication, confidence and problem-solving.

It was the first practical step of the Bootcamp—moving from discussion to presentation, and creating a foundation for the hands-on technology sessions that followed.

Day One had begun with an important lesson: ideas become more powerful when they are shared, challenged and developed together.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, ameagwa rasmi na Menejimenti ya Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zilizo chini yake katika hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Kambarage Treasury Square, Dodoma. Jumatano Septemba 09, 2026.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati anayeshughukia Umeme na Nishati Jadidifu, Mhandisi Felchesmi Mramba, Menejimenti ya Wizara na Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Makamu wa Rais amewaasa Viongozi na Watendaji hao kuendelea kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Wasaidizi wake ili waendelee kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia Watanzania.

Aidha, Makamu wa Rais amewataka Viongozi na Watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi, uaminifu na uzalendo ili kutimiza matarajio ya wananchi kwa Serikali.












Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo, amesema ataendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji ili kukuza uwekezaji na uchumi wa Mkoa wa Pwani, huku akisisitiza umuhimu wa kuwawezesha vijana kiuchumi.

Mhe. Nyongo amesema hayo leo, Septemba 8, 2026, wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani kati yake na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Abubakar Mussa Kunenge, ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Songwe.

Amesema Mkoa wa Pwani ni miongoni mwa maeneo muhimu kwa uwekezaji nchini na kwamba atashirikiana na viongozi na wadau mbalimbali kuhakikisha mazingira yanaendelea kuwa rafiki kwa wawekezaji.

“Mkoa huu ni wa uwekezaji. Nimezunguka maeneo mbalimbali kutafuta wawekezaji, kwa hiyo niwakaribishe kwa kuweka mazingira wezeshi,” amesema Mhe. Nyongo.

Aidha, Mhe. Nyongo ameomba ushirikiano wa jamii katika kuwajenga na kuwawezesha vijana kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi yanayolenga kuboresha maisha yao na jamii kwa ujumla.

Amesema atashirikiana na viongozi wa Mkoa katika kukuza uchumi kupitia sekta mbalimbali, ikiwemo kilimo, mifugo, uchumi wa buluu pamoja na sekta nyingine za uzalishaji.

“Ninaamini utendaji wetu wa pamoja utatumika kikamilifu katika kuendelea kuwatumikia wananchi kwa kutatua changamoto zao mbalimbali, pamoja na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla,” amesema.

Katika hatua nyingine, Mhe. Nyongo ameomba viongozi na wananchi kutumia sheria, kanuni na taratibu katika kutatua migogoro ya ardhi, akisisitiza umuhimu wa kutumia busara na haki ili kupata suluhisho la kudumu.

Ameahidi kulisimamia kwa karibu suala hilo kwa lengo la kuhakikisha migogoro ya ardhi inapungua na wananchi wanapata haki na fursa ya kuendelea na shughuli zao za kiuchumi.

Mheshimiwa Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) akimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026 kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Afrika CDC) Dkt. Jean Kaseya akimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

Mtume Boniface Mwamposa pamoja na Mchungaji Tony Kapola wakimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.
Na Mwandishi Wetu.

ALGIERS: Tanzania na Algeria zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza uzalishaji wa bidhaa hizo na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na la Afrika.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda vya Dawa wa Algeria, Dkt. Wassim Kouidri, katika ofisi za wizara hiyo jijini Algiers.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Matinyi alimweleza Waziri Kouidri kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuendeleza sekta ya viwanda vya dawa, ikiwemo kuweka vivutio maalum kwa wawekezaji.

Alisema tayari viwanda vitano vya dawa vinaendelea kujengwa nchini, huku vingine vikitazamiwa kuanzishwa katika kipindi kijacho.

“Serikali imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha viwanda vya dawa na vifaa vya tiba katika ukanda wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wenye watu takriban milioni 350,” alisema Balozi Matinyi.

Kwa upande wake, Waziri Kouidri aliahidi ushirikiano wa Serikali ya Algeria katika kuisaidia Tanzania kupata utaalamu wa kisasa wa utengenezaji wa dawa na vifaa tiba.

“Ni kweli, Tanzania ipo kwenye eneo zuri la kimkakati la ukanda mkubwa wa Afrika na Algeria iko tayari kushirikiana nayo kitaalamu ili kuhakikisha inafikia malengo yake,” alisema.

Aidha, Balozi Matinyi alikaribisha ziara ya Mamlaka ya Taifa ya Bidhaa za Dawa ya Algeria (ANPP), inayotarajiwa nchini Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu kwa mwaliko wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA).

Ziara hiyo inalenga kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano wa kitaalamu kati ya mamlaka hizo katika sekta ya dawa.

Tanzania pia imeendelea kujijengea heshima barani Afrika katika udhibiti wa dawa baada ya kuwa nchi ya kwanza barani humo kufikia kiwango cha daraja la tatu la ukaguzi wa dawa (ML3) mwaka 2018, chini ya tathmini ya viwango vya Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kiwango hicho hupima ubora na ufanisi wa mifumo ya udhibiti na ukaguzi wa dawa katika nchi.

Tangu mwaka 2020, nchi nyingine tisa za Afrika zimefikia kiwango cha ML3. Nchi hizo ni Afrika Kusini, Ethiopia, Ghana, Misri, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal na Zimbabwe.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna nchi ya Afrika iliyofikia kiwango cha juu zaidi cha ML4.

Kwa upande wa Algeria, nchi hiyo ni miongoni mwa vinara wa sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba barani Afrika ikiwa na viwanda 230, sawa na takriban theluthi moja ya viwanda 690 vilivyopo barani humo.

Ushirikiano huo unatarajiwa kusaidia Tanzania kuongeza uwezo wa uzalishaji wa dawa na vifaa tiba, kupunguza utegemezi wa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje na kuongeza nafasi ya nchi katika soko la dawa la Afrika.
Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Evariste Ndayishimiye, akimfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba 2026, kufuatia kifo cha mume wake, Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan.

Na Mwandishi Wetu.

DAR ES SALAAM: Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amewapongeza walimu wa Kata ya Ukonga kwa mchango wao katika jamii, akisema wamekuwa msingi muhimu wa uzalishaji wa wataalamu na viongozi mbalimbali nchini.

Mhe. Mpogolo ameyasema hayo wakati wa sherehe ya walimu wa Kata ya Ukonga, inayojulikana kama UKONGA DAY, iliyofanyika Ukonga jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mpogolo amesema walimu wana nafasi kubwa katika maendeleo ya Taifa kwa kuwa ndio wanaowaandaa wanafunzi kuwa wataalamu na viongozi wanaokuja kuliongoza na kulitumikia Taifa.
Amesema mchango wa walimu hauishii darasani pekee, bali unaendelea kuonekana kupitia mafanikio ya wanafunzi wao katika nyanja mbalimbali za maisha.

Mhe. Mpogolo ametoa pongezi hizo kufuatia hotuba ya utangulizi iliyotolewa na mgeni maalum wa hafla hiyo, Mhe. Jerry Silaa, ambaye pia ni mlezi wa walimu wa Kata ya Ukonga.

Mhe. Silaa ana historia ya kipekee na eneo hilo, kwani amezaliwa katika Kata ya Ukonga na kusoma katika Shule ya Msingi Ukonga.
Katika safari yake ya maisha, amekuwa akirejea katika eneo hilo na kutoa shukrani kwa walimu wa Kata ya Ukonga, akiwatambua kuwa miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa mafanikio yake.

Aidha, Mhe. Mpogolo amesema walimu ni miongoni mwa watu wanaofurahia mafanikio ya wale waliowafundisha, akieleza kuwa mafanikio ya mwanafunzi ni sehemu ya mafanikio ya mwalimu.

Amesema tofauti na baadhi ya watu ambao wanaweza kuwa na wivu wanapowaona wenzao wakifanikiwa, walimu hufurahia kuona wanafunzi wao wakipiga hatua na kufikia mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mpogolo, hali hiyo inaonesha umuhimu wa kutambua na kuthamini mchango wa walimu katika kujenga jamii na Taifa kwa ujumla.

DODOMA, September 8, 2026:

Efforts to prepare Tanzanian girls for the rapidly expanding digital economy are taking a new direction, with UNESCO calling for gender to be placed at the centre of digital skills education to ensure that girls are not left behind in the country’s digital transformation.

The call comes as Tanzania, through collaboration with UNESCO and Beijing Normal University (BNU), implements the “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls” project, an initiative aimed at strengthening digital skills while addressing barriers that continue to limit girls’ participation in technology and innovation.

Gender specialist Dr Rosemarie N. Mwaipopo said digitalisation was no longer simply a matter of access to computers or the internet, but an increasingly important pathway to education, employment, innovation and wider socio-economic development.

She said the country’s digital transformation would have greater impact if girls were given deliberate opportunities to acquire digital skills, participate in innovation and develop the confidence needed to pursue technology-related education and careers.

“Digitalisation is a major influence in societal development, enhancing access to opportunities,” Dr Mwaipopo said, while emphasising the need to confront the persistent gender gap in digital participation.

She questioned why the gap continued to exist globally and in Tanzania despite various innovations, programmes and interventions designed to expand access to technology and digital skills.

According to her, the challenge was not only about whether technology was available, but also about who had the skills, confidence, opportunity and enabling environment to use that technology and turn it into meaningful solutions.

She said this was where the UNESCO-BNU project could make an important contribution by introducing a gender perspective into digital skills education.

CREATING A CRITICAL MASS OF GIRLS IN ICT

Dr Mwaipopo said the project would deliberately select female students to participate in ICT innovation training as part of an affirmative action approach aimed at creating a critical mass of girls with digital knowledge and skills.
She said increasing the number of girls exposed to technology and innovation would help challenge the long-standing perception that ICT and STEM-related fields were predominantly for boys.

The approach, she explained, was intended to create more girls who could confidently engage with technology, develop innovations and eventually pursue careers in the digital sector.

“This is not simply about teaching girls how to use technology. It is about creating opportunities for them to become knowledgeable, confident and active participants in the digital future,” she said.
She said a growing pool of digitally skilled girls could also provide role models for younger generations and contribute to changing community perceptions about the role of women in technology.

CHANGING THE WAY GIRLS LEARN

Dr Mwaipopo said teachers would be equally important in achieving this transformation.

She called for teachers to be equipped with gender-transformative pedagogy, enabling them to recognise and challenge attitudes, practices and social norms that may discourage girls from participating fully in ICT and STEM education.

She said teachers needed to create classrooms where girls felt confident to experiment, ask questions, solve problems and develop technological innovations.

The objective, she said, was to move beyond simply providing equal access to boys and girls towards creating learning environments capable of transforming the conditions that have historically limited girls’ participation.

She said teachers and students would also need greater awareness of gender equality, gender barriers, enabling factors and intersectionality to understand why girls may experience digital education differently depending on their social and economic circumstances.

INNOVATION THAT WORKS FOR EVERYONE

Dr Mwaipopo further challenged students to think about gender when developing ICT solutions.
She said female students should be equipped to apply a gender lens in ICT processes and innovation, ensuring that digital products and solutions were accessible, sensitive to different needs and inclusive.

She explained that successful digital innovation should not only answer the question of whether a technology works, but also consider who can access it, who can use it and who ultimately benefits from it.

Such an approach, she said, would enable girls to see technology as more than computers and coding, but as a powerful tool for addressing real challenges facing families, communities and the country.

BUILDING TANZANIA’S DIGITAL GENERATION

The gender-transformative approach is being implemented alongside efforts to establish and strengthen ICT Clubs in public schools, providing girls with practical opportunities to develop digital skills, participate in innovation and explore technology-related career pathways.

The broader UNESCO-BNU initiative is being implemented in collaboration with the Government of the United Republic of Tanzania, reflecting the importance of partnerships in strengthening digital education and expanding opportunities for women and girls.

Through the project, teachers and female students are expected to gain skills and approaches that can contribute to more inclusive digital learning environments.

For Tanzania, the initiative comes at a time when digital skills are increasingly becoming essential for education, employment, entrepreneurship and innovation.
Its significance therefore extends beyond the classroom.

By deliberately investing in girls’ digital skills today, the country is building a generation capable of participating in and contributing to tomorrow’s technology-driven economy.

The ultimate ambition is to ensure that Tanzanian girls are not merely users of technology, but creators, innovators, entrepreneurs and future leaders in the digital economy.

And by ensuring that no girl is excluded from the digital transformation, Tanzania can strengthen its human capital and build a more inclusive digital future in which every girl has an opportunity to learn, innovate and shape the country’s development.
Washindi wa Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament katika makundi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea zawadi zao, Tukio hilo lilifanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando (kushoto), akikabidhi zawadi ya tiketi ya kwenda na kurudi Mauritius kwa mshindi wa jumla kwa wanaume Khalid Shemndolwa (wa tatu kushoto) katika mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Shemndolwa alikusanya point 42 katika mashindano yaliyoshirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.
Mshindi wa jumla kwa upande wa wanawake, Yvonne Ondari (wa tatu kushoto), akipokea zawadi baada ya kutwaa taji katika Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament yaliyofanyika Lugalo Golf Club mwishoni mwa wiki. Ondari alikusanya pointi 42 (CB) katika mashindano yaliyoshirikisha wachezaji golf 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, akishiriki mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, Septemba 5, 2026. Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Business Joseph Sayi, akishiriki mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, Septemba 5, 2026. Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es salaam, Septemba 5, 2026:  Vodacom Tanzania PLC, kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited, imehitimisha mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yaliyofanyika katika Uwanja wa TPDF Lugalo Golf Club, yakiwakutanisha wachezaji wapatao 150 kutoka Tanzania na nchi jirani, wakiwemo viongozi wa biashara, wakurugenzi na wakuu wa makampuni pamoja na wapenzi wa mchezo wa golf.

Wachezaji gofu Khalid Shemndolwa na Yvonne Ondari wameibuka washinda kwa jumla shindano la Vodacom Corporate Masters kwa upande wa wanaume na wanawake. Katika shindano hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Lugalo, Shemndolwa alikusanya pointi 42 huku Ondari akikusanya pointi kama hizo katika mashindano hayo ya siku moja. 

Mbali ya Shemndolwa na Ondari, Godfrey Abel aliibuka mhsindi katika daraja A, kwa kupata pointi 42, akifuatiwa na Likuli Juma aliyepata pointi 41 ambapo Sigfrid Urassa alitwaa ubingwa wa daraja B kwa pointi 40, akimzidi Godfrey Kilenga aliyemaliza na pointi hizo hizo, lakini Urassa akashinda kwa kanuni ya countback.

Boniface Japhet alitwaa ubingwa wa daraha C  baada ya kupata pointi 39, huku Abdallah Singano akimaliza nafasi ya pili kwa pointi 37. Kwa upande wa wanawake, Neema Job alimaliza na pointi 42 na kutwaa ubingwa, akifuatiwa na Leticia Kapalia aliyepata pointi 40. Mashindano ya timu za kampuni nayo yalikuwa kivutio kikubwa, huku timu ya KQ ikiibuka mshindi baada ya kushindana na timu nyingine tisa za kampuni.

Zawadi maalum za mtu mmoja mmoja zilienda kwa Michael Norbert aliyeshinda Longest Drive kwa wanaume, huku Kapalia akitwaa tuzo hiyo kwa wanawake. Harshid Barmeda alishinda Nearest to the Pin kwa wanaume, wakati Vaileth James akitwaa tuzo hiyo kwa wanawake.

Mbali na ushindani, washiriki pamoja na familia zao walifurahia shughuli mbalimbali katika eneo la Corporate Village, lililokuwa na burudani, maonesho ya biashara, magari ya zamani pamoja na eneo maalum la watoto.

Mkurugenzi wa Vodacom Business wa Vodacom Tanzania PLC, Nguvu Kamando, alisema mashindano hayo yameendelea kuonyesha nafasi ya michezo katika kujenga mahusiano yenye tija katika biashara.

“Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup imethibitisha tena kwamba michezo ni jukwaa lenye nguvu katika kujenga mahusiano ya muda mrefu ya kibiashara. Tunafurahishwa na ushiriki mkubwa wa kampuni na kasi ya mahusiano mapya yaliyojengwa wiki hii,” alisema Kamando.

Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Kariuki, alizipongeza kampuni zilizoshiriki na kusema mashindano hayo yanaendelea kuchangia katika kujenga mtandao wa kibiashara na kukuza mchezo wa gofu.“Mwaka huu tulishuhudia ushindani wa kiwango cha juu uwanjani na ushiriki wenye maana katika biashara nje ya uwanja. Hilo ndilo lengo kuu la Corporate Masters, kuzikutanisha kampuni katika mazingira rafiki yanayozalisha fursa halisi za ushirikiano,” alisema Kariuki.

Alisema ushirikiano kati ya Vodacom na Corporate Masters unaonyesha namna kampuni zinavyoweza kufanya kazi pamoja katika kutengeneza thamani kwa wateja na wadau, huku zikiunga mkono maendeleo ya mchezo wa gofu nchini Tanzania.

Kufanikiwa kwa mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 kunaendelea kuthibitisha mkakati wa Vodacom Tanzania wa kutumia michezo kama jukwaa la kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kuhamasisha ubunifu na kuwasogeza karibu viongozi wa biashara na suluhisho za kidijitali zinazochochea ukuaji wa uchumi wa Tanzania.