TRENDING NOW





Mheshimiwa Felix Antoine Tshisekedi Tshilombo, Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) akimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026 kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Afrika CDC) Dkt. Jean Kaseya akimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.

Mtume Boniface Mwamposa pamoja na Mchungaji Tony Kapola wakimfariji Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuwasili nyumbani kwake Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, tarehe 08 Septemba, 2026, kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena Zanzibar, tarehe 07 Sept, 2026.
Na Mwandishi Wetu.

ALGIERS: Tanzania na Algeria zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuongeza uzalishaji wa bidhaa hizo na kukidhi mahitaji ya soko la ndani na la Afrika.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya Balozi wa Tanzania nchini Algeria, Mhe. Mobhare Matinyi, kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Viwanda vya Dawa wa Algeria, Dkt. Wassim Kouidri, katika ofisi za wizara hiyo jijini Algiers.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Matinyi alimweleza Waziri Kouidri kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuendeleza sekta ya viwanda vya dawa, ikiwemo kuweka vivutio maalum kwa wawekezaji.

Alisema tayari viwanda vitano vya dawa vinaendelea kujengwa nchini, huku vingine vikitazamiwa kuanzishwa katika kipindi kijacho.

“Serikali imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha viwanda vya dawa na vifaa vya tiba katika ukanda wa nchi za mashariki, kati na kusini mwa Afrika wenye watu takriban milioni 350,” alisema Balozi Matinyi.

Kwa upande wake, Waziri Kouidri aliahidi ushirikiano wa Serikali ya Algeria katika kuisaidia Tanzania kupata utaalamu wa kisasa wa utengenezaji wa dawa na vifaa tiba.

“Ni kweli, Tanzania ipo kwenye eneo zuri la kimkakati la ukanda mkubwa wa Afrika na Algeria iko tayari kushirikiana nayo kitaalamu ili kuhakikisha inafikia malengo yake,” alisema.

Aidha, Balozi Matinyi alikaribisha ziara ya Mamlaka ya Taifa ya Bidhaa za Dawa ya Algeria (ANPP), inayotarajiwa nchini Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu kwa mwaliko wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA).

Ziara hiyo inalenga kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano wa kitaalamu kati ya mamlaka hizo katika sekta ya dawa.

Tanzania pia imeendelea kujijengea heshima barani Afrika katika udhibiti wa dawa baada ya kuwa nchi ya kwanza barani humo kufikia kiwango cha daraja la tatu la ukaguzi wa dawa (ML3) mwaka 2018, chini ya tathmini ya viwango vya Shirika la Afya Duniani (WHO).

Kiwango hicho hupima ubora na ufanisi wa mifumo ya udhibiti na ukaguzi wa dawa katika nchi.

Tangu mwaka 2020, nchi nyingine tisa za Afrika zimefikia kiwango cha ML3. Nchi hizo ni Afrika Kusini, Ethiopia, Ghana, Misri, Msumbiji, Nigeria, Rwanda, Senegal na Zimbabwe.

Hata hivyo, hadi sasa hakuna nchi ya Afrika iliyofikia kiwango cha juu zaidi cha ML4.

Kwa upande wa Algeria, nchi hiyo ni miongoni mwa vinara wa sekta ya viwanda vya dawa na vifaa tiba barani Afrika ikiwa na viwanda 230, sawa na takriban theluthi moja ya viwanda 690 vilivyopo barani humo.

Ushirikiano huo unatarajiwa kusaidia Tanzania kuongeza uwezo wa uzalishaji wa dawa na vifaa tiba, kupunguza utegemezi wa bidhaa zinazoagizwa kutoka nje na kuongeza nafasi ya nchi katika soko la dawa la Afrika.
Na Mwandishi Wetu.

DAR ES SALAAM: Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mhe. Edward Mpogolo, amewapongeza walimu wa Kata ya Ukonga kwa mchango wao katika jamii, akisema wamekuwa msingi muhimu wa uzalishaji wa wataalamu na viongozi mbalimbali nchini.

Mhe. Mpogolo ameyasema hayo wakati wa sherehe ya walimu wa Kata ya Ukonga, inayojulikana kama UKONGA DAY, iliyofanyika Ukonga jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Mpogolo amesema walimu wana nafasi kubwa katika maendeleo ya Taifa kwa kuwa ndio wanaowaandaa wanafunzi kuwa wataalamu na viongozi wanaokuja kuliongoza na kulitumikia Taifa.
Amesema mchango wa walimu hauishii darasani pekee, bali unaendelea kuonekana kupitia mafanikio ya wanafunzi wao katika nyanja mbalimbali za maisha.

Mhe. Mpogolo ametoa pongezi hizo kufuatia hotuba ya utangulizi iliyotolewa na mgeni maalum wa hafla hiyo, Mhe. Jerry Silaa, ambaye pia ni mlezi wa walimu wa Kata ya Ukonga.

Mhe. Silaa ana historia ya kipekee na eneo hilo, kwani amezaliwa katika Kata ya Ukonga na kusoma katika Shule ya Msingi Ukonga.
Katika safari yake ya maisha, amekuwa akirejea katika eneo hilo na kutoa shukrani kwa walimu wa Kata ya Ukonga, akiwatambua kuwa miongoni mwa watu waliochangia kwa kiasi kikubwa mafanikio yake.

Aidha, Mhe. Mpogolo amesema walimu ni miongoni mwa watu wanaofurahia mafanikio ya wale waliowafundisha, akieleza kuwa mafanikio ya mwanafunzi ni sehemu ya mafanikio ya mwalimu.

Amesema tofauti na baadhi ya watu ambao wanaweza kuwa na wivu wanapowaona wenzao wakifanikiwa, walimu hufurahia kuona wanafunzi wao wakipiga hatua na kufikia mafanikio makubwa.

Kwa mujibu wa Mhe. Mpogolo, hali hiyo inaonesha umuhimu wa kutambua na kuthamini mchango wa walimu katika kujenga jamii na Taifa kwa ujumla.

DODOMA, September 8, 2026:

Efforts to prepare Tanzanian girls for the rapidly expanding digital economy are taking a new direction, with UNESCO calling for gender to be placed at the centre of digital skills education to ensure that girls are not left behind in the country’s digital transformation.

The call comes as Tanzania, through collaboration with UNESCO and Beijing Normal University (BNU), implements the “Closing the Digital Divide: Ensuring Gender-Transformative Digital Skills Education for Women and Girls” project, an initiative aimed at strengthening digital skills while addressing barriers that continue to limit girls’ participation in technology and innovation.

Gender specialist Dr Rosemarie N. Mwaipopo said digitalisation was no longer simply a matter of access to computers or the internet, but an increasingly important pathway to education, employment, innovation and wider socio-economic development.

She said the country’s digital transformation would have greater impact if girls were given deliberate opportunities to acquire digital skills, participate in innovation and develop the confidence needed to pursue technology-related education and careers.

“Digitalisation is a major influence in societal development, enhancing access to opportunities,” Dr Mwaipopo said, while emphasising the need to confront the persistent gender gap in digital participation.

She questioned why the gap continued to exist globally and in Tanzania despite various innovations, programmes and interventions designed to expand access to technology and digital skills.

According to her, the challenge was not only about whether technology was available, but also about who had the skills, confidence, opportunity and enabling environment to use that technology and turn it into meaningful solutions.

She said this was where the UNESCO-BNU project could make an important contribution by introducing a gender perspective into digital skills education.

CREATING A CRITICAL MASS OF GIRLS IN ICT

Dr Mwaipopo said the project would deliberately select female students to participate in ICT innovation training as part of an affirmative action approach aimed at creating a critical mass of girls with digital knowledge and skills.
She said increasing the number of girls exposed to technology and innovation would help challenge the long-standing perception that ICT and STEM-related fields were predominantly for boys.

The approach, she explained, was intended to create more girls who could confidently engage with technology, develop innovations and eventually pursue careers in the digital sector.

“This is not simply about teaching girls how to use technology. It is about creating opportunities for them to become knowledgeable, confident and active participants in the digital future,” she said.
She said a growing pool of digitally skilled girls could also provide role models for younger generations and contribute to changing community perceptions about the role of women in technology.

CHANGING THE WAY GIRLS LEARN

Dr Mwaipopo said teachers would be equally important in achieving this transformation.

She called for teachers to be equipped with gender-transformative pedagogy, enabling them to recognise and challenge attitudes, practices and social norms that may discourage girls from participating fully in ICT and STEM education.

She said teachers needed to create classrooms where girls felt confident to experiment, ask questions, solve problems and develop technological innovations.

The objective, she said, was to move beyond simply providing equal access to boys and girls towards creating learning environments capable of transforming the conditions that have historically limited girls’ participation.

She said teachers and students would also need greater awareness of gender equality, gender barriers, enabling factors and intersectionality to understand why girls may experience digital education differently depending on their social and economic circumstances.

INNOVATION THAT WORKS FOR EVERYONE

Dr Mwaipopo further challenged students to think about gender when developing ICT solutions.
She said female students should be equipped to apply a gender lens in ICT processes and innovation, ensuring that digital products and solutions were accessible, sensitive to different needs and inclusive.

She explained that successful digital innovation should not only answer the question of whether a technology works, but also consider who can access it, who can use it and who ultimately benefits from it.

Such an approach, she said, would enable girls to see technology as more than computers and coding, but as a powerful tool for addressing real challenges facing families, communities and the country.

BUILDING TANZANIA’S DIGITAL GENERATION

The gender-transformative approach is being implemented alongside efforts to establish and strengthen ICT Clubs in public schools, providing girls with practical opportunities to develop digital skills, participate in innovation and explore technology-related career pathways.

The broader UNESCO-BNU initiative is being implemented in collaboration with the Government of the United Republic of Tanzania, reflecting the importance of partnerships in strengthening digital education and expanding opportunities for women and girls.

Through the project, teachers and female students are expected to gain skills and approaches that can contribute to more inclusive digital learning environments.

For Tanzania, the initiative comes at a time when digital skills are increasingly becoming essential for education, employment, entrepreneurship and innovation.
Its significance therefore extends beyond the classroom.

By deliberately investing in girls’ digital skills today, the country is building a generation capable of participating in and contributing to tomorrow’s technology-driven economy.

The ultimate ambition is to ensure that Tanzanian girls are not merely users of technology, but creators, innovators, entrepreneurs and future leaders in the digital economy.

And by ensuring that no girl is excluded from the digital transformation, Tanzania can strengthen its human capital and build a more inclusive digital future in which every girl has an opportunity to learn, innovate and shape the country’s development.
Washindi wa Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament katika makundi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kupokea zawadi zao, Tukio hilo lilifanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando (kushoto), akikabidhi zawadi ya tiketi ya kwenda na kurudi Mauritius kwa mshindi wa jumla kwa wanaume Khalid Shemndolwa (wa tatu kushoto) katika mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Shemndolwa alikusanya point 42 katika mashindano yaliyoshirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.
Mshindi wa jumla kwa upande wa wanawake, Yvonne Ondari (wa tatu kushoto), akipokea zawadi baada ya kutwaa taji katika Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Tournament yaliyofanyika Lugalo Golf Club mwishoni mwa wiki. Ondari alikusanya pointi 42 (CB) katika mashindano yaliyoshirikisha wachezaji golf 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, akishiriki mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, Septemba 5, 2026. Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Business Joseph Sayi, akishiriki mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup yaliyofanyika Lugalo Golf Club, Dar es Salaam, Septemba 5, 2026. Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji gofu 150 kutoka Tanzania na nje ya nchi.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es salaam, Septemba 5, 2026:  Vodacom Tanzania PLC, kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited, imehitimisha mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yaliyofanyika katika Uwanja wa TPDF Lugalo Golf Club, yakiwakutanisha wachezaji wapatao 150 kutoka Tanzania na nchi jirani, wakiwemo viongozi wa biashara, wakurugenzi na wakuu wa makampuni pamoja na wapenzi wa mchezo wa golf.

Wachezaji gofu Khalid Shemndolwa na Yvonne Ondari wameibuka washinda kwa jumla shindano la Vodacom Corporate Masters kwa upande wa wanaume na wanawake. Katika shindano hilo lililofanyika kwenye uwanja wa Lugalo, Shemndolwa alikusanya pointi 42 huku Ondari akikusanya pointi kama hizo katika mashindano hayo ya siku moja. 

Mbali ya Shemndolwa na Ondari, Godfrey Abel aliibuka mhsindi katika daraja A, kwa kupata pointi 42, akifuatiwa na Likuli Juma aliyepata pointi 41 ambapo Sigfrid Urassa alitwaa ubingwa wa daraja B kwa pointi 40, akimzidi Godfrey Kilenga aliyemaliza na pointi hizo hizo, lakini Urassa akashinda kwa kanuni ya countback.

Boniface Japhet alitwaa ubingwa wa daraha C  baada ya kupata pointi 39, huku Abdallah Singano akimaliza nafasi ya pili kwa pointi 37. Kwa upande wa wanawake, Neema Job alimaliza na pointi 42 na kutwaa ubingwa, akifuatiwa na Leticia Kapalia aliyepata pointi 40. Mashindano ya timu za kampuni nayo yalikuwa kivutio kikubwa, huku timu ya KQ ikiibuka mshindi baada ya kushindana na timu nyingine tisa za kampuni.

Zawadi maalum za mtu mmoja mmoja zilienda kwa Michael Norbert aliyeshinda Longest Drive kwa wanaume, huku Kapalia akitwaa tuzo hiyo kwa wanawake. Harshid Barmeda alishinda Nearest to the Pin kwa wanaume, wakati Vaileth James akitwaa tuzo hiyo kwa wanawake.

Mbali na ushindani, washiriki pamoja na familia zao walifurahia shughuli mbalimbali katika eneo la Corporate Village, lililokuwa na burudani, maonesho ya biashara, magari ya zamani pamoja na eneo maalum la watoto.

Mkurugenzi wa Vodacom Business wa Vodacom Tanzania PLC, Nguvu Kamando, alisema mashindano hayo yameendelea kuonyesha nafasi ya michezo katika kujenga mahusiano yenye tija katika biashara.

“Vodacom Corporate Masters 2026 Golf Cup imethibitisha tena kwamba michezo ni jukwaa lenye nguvu katika kujenga mahusiano ya muda mrefu ya kibiashara. Tunafurahishwa na ushiriki mkubwa wa kampuni na kasi ya mahusiano mapya yaliyojengwa wiki hii,” alisema Kamando.

Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Kariuki, alizipongeza kampuni zilizoshiriki na kusema mashindano hayo yanaendelea kuchangia katika kujenga mtandao wa kibiashara na kukuza mchezo wa gofu.“Mwaka huu tulishuhudia ushindani wa kiwango cha juu uwanjani na ushiriki wenye maana katika biashara nje ya uwanja. Hilo ndilo lengo kuu la Corporate Masters, kuzikutanisha kampuni katika mazingira rafiki yanayozalisha fursa halisi za ushirikiano,” alisema Kariuki.

Alisema ushirikiano kati ya Vodacom na Corporate Masters unaonyesha namna kampuni zinavyoweza kufanya kazi pamoja katika kutengeneza thamani kwa wateja na wadau, huku zikiunga mkono maendeleo ya mchezo wa gofu nchini Tanzania.

Kufanikiwa kwa mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 kunaendelea kuthibitisha mkakati wa Vodacom Tanzania wa kutumia michezo kama jukwaa la kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kuhamasisha ubunifu na kuwasogeza karibu viongozi wa biashara na suluhisho za kidijitali zinazochochea ukuaji wa uchumi wa Tanzania.

Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN), Beda Msimbe (Kushoto) akizungumza mara baada ya kupokea timu ya maofisa wa PSSSF ilipotembelea Makao Makuu ya Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) yaliyopo Kijitonyama, Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Msafara wa PSSSF, Abdul Njaidi.

Na Mwandishi Wetu TBN, DAR ES SALAAM.

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umeeleza dhamira ya kutumia nguvu ya majukwaa ya kidijitali kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa elimu kuhusu hifadhi ya jamii, pensheni na uwekezaji, kupitia ushirikiano na Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN).

Ushirikiano huo umejadiliwa wakati timu ya maofisa wa PSSSF ilipotembelea Makao Makuu ya Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) yaliyopo Kijitonyama, Dar es Salaam, ambapo pande hizo zilikubaliana kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa taarifa sahihi na uelimishaji wa umma.

Mwenyekiti wa TBN, Beda Msimbe, alisema mtandao huo wenye zaidi ya wanachama 200 nchini na Diaspora una nafasi kubwa ya kusaidia taasisi mbalimbali kuwafikia wananchi kupitia majukwaa ya kidijitali.

Msimbe alisema TBN iko tayari kutumia mtandao wake katika kuelimisha jamii kuhusu huduma na shughuli za PSSSF, huku akisisitiza umuhimu wa wanablogu kupata mafunzo ya kina kuhusu masuala ya hifadhi ya jamii ili taarifa wanazozifikisha kwa umma ziwe sahihi na zenye uelewa mpana.

Kwa upande wake, Mkuu wa Msafara wa PSSSF, Abdul Njaidi, alisema ushirikiano huo ni sehemu ya jitihada za mfuko kuimarisha uhusiano na wadau wa habari ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu kwa jamii.

Njaidi alisema mapendekezo na hoja zilizowasilishwa na TBN zitafanyiwa kazi, akisisitiza kuwa PSSSF inalenga kuhakikisha wananchi wanaelewa kwa usahihi masuala ya pensheni, hifadhi ya jamii na uwekezaji unaofanywa na mfuko huo.
Naye Mdhamini wa TBN, Issa Michuzi, alisema mtandao huo una uzoefu mkubwa katika uandishi na usambazaji wa habari za kidijitali na uko tayari kushirikiana na PSSSF katika kuhakikisha elimu ya hifadhi ya jamii inawafikia wananchi kwa lugha rahisi na inayoeleweka.

Alisema TBN imejengwa kwa dhamira ya kukuza mazingira bora ya habari za kidijitali nchini, hivyo ushirikiano huo unaweza kuwa chachu ya kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu masuala yanayogusa maisha na ustawi wao wa baadaye.
Katibu wa TBN, Rahel Pallangyo, alisema majukwaa ya wanachama wa mtandao huo yanaweza kuwa kiungo muhimu kati ya PSSSF na wananchi, hasa katika kipindi ambacho mitandao ya kidijitali imekuwa chanzo muhimu cha habari na maarifa.

Ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa taarifa sahihi kuhusu hifadhi ya jamii, pensheni na fursa za uwekezaji, huku ukilenga kuwafikia wananchi wengi zaidi ndani na nje ya Tanzania.

Ujumbe wa PSSSF uliongozwa na Abdul Njaidi na kuwajumuisha Regina Kumba, Grayson Mgunda na Doreen Lyimo, huku upande wa TBN ukihudhuriwa na Mwenyekiti Beda Msimbe, Katibu Rahel Pallangyo, Mtaalamu wa Mawasiliano Cathbert Kajuna na Mdhamini Issa Michuzi.

Kilimanjaro-Tanzania: Kampuni ya Bia Serengeti (SBL) imeeleza mchango wa uwekezaji wa sekta binafsi katika mageuzi ya kiuchumi ya Tanzania wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumi ya Bunge ya Bajeti katika kiwanda chake Kilimanjaro-Moshi.

Ziara hiyo ilitoa fursa kwa kamati kujionea moja kwa moja uwekezaji wa SBL nchini Tanzania, mchango wake katika sekta ya viwanda na uchumi kwa ujumla, pamoja na hatua zinazounga mkono kilimo cha ndani, ajira, maendeleo ya ujuzi, jamii na uendelevu wa mazingira.

Mkutano huo umefanyika wakati Tanzania ikiendelea kutekeleza Dira 2050, ambayo inatambua sekta binafsi imara na yenye nguvu kama kichocheo muhimu cha mageuzi ya kiuchumi, tija, ubunifu, uwekezaji na uundwaji wa ajira.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Dkt. Obinna Anyalebechi, alisema SBL inaona uwekezaji wake nchini Tanzania ukienda mbali zaidi ya shughuli zake za uzalishaji hadi kufikia mnyororo mzima wa thamani na jamii inazofanya nazo kazi.

"Tanzania inapoelekea 2050, sekta binafsi ina jukumu muhimu la kuhakikisha matarajio ya Dira 2050 ya nchi yetu yanageuka kuwa matokeo halisi. Kwa hiyo tumefurahi kuwakaribisha wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti katika Kiwanda chetu cha Moshi na kuonyesha moja kwa moja uwekezaji tunaoufanya katika uzalishaji wa ndani, watu wetu, na mnyororo mpana wa thamani. Katika SBL, tunaendelea kujitolea kufanya kazi kwa ushirikiano na Serikali kuunga mkono ajenda ya viwanda ya Tanzania, kujenga na kuongeza ajira, kuimarisha minyororo ya thamani ya ndani, na kuchangia ukuaji endelevu wa kiuchumi," alisema Dkt. Anyalebechi.

Kwa miaka mingi, SBL imeendelea kuwekeza katika mnyororo wake wa thamani na katika mipango inayounga mkono vipaumbele vya maendeleo vya Tanzania. Kupitia mpango wake wa Shamba ni Mali, kampuni inasaidia wakulima wadogo wanaolima mazao muhimu ikiwemo mtama, shayiri na mahindi, ikiwa na lengo la kufikia wakulima 10,000 ifikapo mwaka 2030. Mpango huu unalenga kuimarisha tija ya kilimo huku ukijenga uhusiano thabiti zaidi kati ya kilimo cha ndani na uzalishaji viwandani.

Katika ziara hiyo SBL pia ilieleza kuwa imewekeza katika jamii kupitia mpango wake wa ‘Water for Life’. Tangu mwaka 2010, kampuni imetekeleza miradi 32 ya maji yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 2, nakunufaisha zaidi ya Watanzania milioni mbili wanaoishi vijijini kwa kuwapatia maji safi na salama. Uwekezaji huu unaonyesha dhamira ya kampuni katika kushughulikia mahitaji ya jamii huku ikisaidia ustawi wa jamii na uchumi wa muda mrefu.

Aidha, kupitia mpango wake wa ‘Learning for Life’, unaotekelezwa kwa ushirikiano na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT), SBL imewasaidia vijana wa Kitanzania kupata ujuzi katika sekta ya hoteli na utalii unaolenga kuboresha nafasi zao za ajira na kuimarisha mnyororo wa thamani wa utalii na ukarimu nchini.Uendelevu unaendelea kuwa kiini cha mkakati wa uwekezaji wa muda mrefu wa SBL, huku kampuni ikiendelea kuzingatia matumizi bora ya maji, kilimo endelevu, nishati jadidifu, ufungashaji wa bidhaa na hatua nyingine zinazolenga kupunguza athari zake za kimazingira huku ikijenga biashara imara.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti Mhe. Mashimba Ndaki, alisema mkutano huo ulikuwa muhimu katika kuimarisha ushirikiano  kati ya Bunge na sekta binafsi na kutambua mchango wa biashara katika kuunga mkono ajenda ya maendeleo ya Tanzania.

"Ziara hii imetoa fursa ya kuelewa moja kwa moja mchango wa uwekezaji wa sekta binafsi katika uzalishaji viwandani, ajira, minyororo ya thamani ya ndani na jamii. Tunapoelekea kutimiza matarajio ya Dira 2050, ushirikiano endelevu kati ya Serikali na sekta binafsi ni muhimu katika kujenga mazingira yanayowezesha uwekezaji, tija na ukuaji endelevu wa uchumi," Mhe. Ndaki.

Ziara hiyo imethibitisha tena umuhimu wa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi katika kusukuma mbele matarajio ya maendeleo ya muda mrefu ya Tanzania. Kwa SBL, ziara hii pia imesisitiza dhamira yake endelevu ya kuwekeza nchini Tanzania na kujenga thamani ya pamoja kupitia watu wake, minyororo ya thamani ya ndani pamoja na jamii kwa ujumla. 



Na Mwandishi Wetu, Tanga

Ujumbe kutoka International Fund for Agricultural Development (IFAD) pamoja na wataalamu kutoka sekta zinazotekeleza Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP), wamekutana mkoani Tanga kwa ajili ya kufanya mapitio ya utekelezaji wa programu hiyo na kutathmini mafanikio yaliyopatikana.

Timu hiyo pia inatarajiwa kutembelea maeneo mbalimbali yanayotekeleza AFDP mkoani Tanga, ikiwemo Kata ya Msomela katika Halmashauri ya Handeni Vijijini, ambako programu imehamasisha jamii ya Kimasai kushiriki katika kilimo bora.

Kupitia programu hiyo, jamii hiyo ambayo kwa asili ni wafugaji imeanza kujihusisha na kilimo cha mahindi chenye tija. Aidha, AFDP imewezesha kuanzishwa kwa mashamba darasa (FFS) kwa ajili ya mazao ya alizeti, mahindi na maharage.

Mashamba hayo yameonyesha mafanikio makubwa, ambapo hekta moja imekuwa na uwezo wa kuzalisha takribani magunia 20 ya mahindi, kila moja likiwa na uzito wa kilogramu 100. Hatua hiyo imewezesha jamii kupata chakula na kuongeza shughuli za kiuchumi kupitia kilimo.

Kwa upande wa sekta ya uvuvi, AFDP inaendelea na ujenzi wa Soko la Kimataifa la Samaki Kipumbwi katika Halmashauri ya Pangani. Ujenzi wa soko hilo umefikia asilimia 68 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2026.

Programu hiyo pia inaendelea na ujenzi wa vichanja 40 vya kukaushia dagaa, ambavyo kwa pamoja vina uwezo wa kukaushia takribani tani tano za dagaa kwa wakati mmoja.

Aidha, AFDP inaendelea na ujenzi wa ghala la baridi pamoja na mtambo wa barafu katika soko hilo, hatua inayolenga kuboresha uhifadhi na usafirishaji wa samaki na kuongeza thamani ya mazao ya uvuvi.

Awali, Mkurugenzi Mkazi wa IFAD nchini, Seth Meng, alikutana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Emmanuel Kisongo, na kufanya mazungumzo kuhusu utekelezaji wa programu hiyo mkoani humo pamoja na mafanikio yanayotarajiwa kwa wananchi wa maeneo yanayonufaika.

Kaimu Katibu Tawala huyo alisema AFDP ni muhimu katika kuchochea maendeleo ya sekta za kilimo na uvuvi mkoani Tanga, huku akiishukuru IFAD kwa juhudi za kuwafikia wananchi na kuomba uwekezaji zaidi uongezwe mkoani humo.

Mkuu wa Idara ya Biashara wa Benki ya Stanbic Tanzania, Fredrick Max (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar, ZEEA, Juma Burhan Mohamed (kulia), wakionesha nakala za Hati ya Makubaliano ya miaka mitano inayolenga kuimarisha ujasiriamali, upatikanaji wa huduma za kifedha na ukuaji endelevu wa biashara Zanzibar. Utiaji saini huo ulishuhudiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdullah, wakati wa Maonyesho ya Fahari ya Zanzibar 2026.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, akishuhudia utiaji saini wa Hati ya Makubaliano ya miaka mitano kati ya Benki ya Stanbic Tanzania na Taasisi ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar, ZEEA, yenye lengo la kuimarisha ujasiriamali, upatikanaji wa huduma za kifedha na ukuaji endelevu wa biashara Zanzibar. Makubaliano hayo yalisainiwa na Mkuu wa Idara ya Biashara wa Benki ya Stanbic Tanzania, Fredrick Max (kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa ZEEA, Juma Burhan Mohamed (kulia0, wakati wa Maonyesho ya Fahari ya Zanzibar 2026.
●Makubaliano haya yatapanua msaada kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo na wa kati walioko Unguja na Pemba.

●Ushirikiano huu unaimarisha jukumu kuu la ZEEA la uwezeshaji wananchi kiuchumi na utaalamu wa kifedha ulioko Stanbic, uendelezaji wa biashara na uunganishaji wa wafanyabiashara na masoko tofauti.

●Utiaji saini huo unafanyika katika Maonyesho ya Fahari ya Zanzibar 2026, ambapo benki ya Stanbic ndiye mdhamini mkuu kwa kuwezesha jumla ya Shilingi milioni 200.

Na Mwandishi Wetu.

Zanzibar, Tanzania – Jumamosi, tarehe 5 Septemba 2026: Benki ya Stanbic Tanzania na Taasisi ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) leo zimesaini Hati ya Makubaliano ya miaka mitano ya kuanzisha ushirikiano wa kimkakati wa kuimarisha ujasiriamali, upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wote na ukuaji endelevu wa biashara Zanzibar.

Makubaliano hayo yalisainiwa wakati wa uzinduzi rasmi wa Maonyesho ya Fahari ya Zanzibar 2026 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, na kushuhudiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdullah.

Kiini cha ushirikiano huu ni nia ya pamoja ya kuzisaidia biashara nyingi zaidi za Zanzibar kutoka katika hatua ya uwezo uliopo na kufikia ukuaji endelevu. Stanbic na ZEEA zitashirikiana kuimarisha elimu ya fedha, urasimishaji wa biashara, upatikanaji wa mitaji, huduma za kifedha za kidijitali, uendelezaji wa biashara pamoja na upatikanaji wa masoko kwa wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo na wa kati katika Unguja na Pemba.

Ushirikiano huu unajengwa juu ya lengo la Fahari ya Zanzibar yenyewe. Maonyesho haya ya kitaifa ya biashara yalianzishwa ili kuvipatia bidhaa na biashara za Zanzibar nafasi ya kufika sokoni, kwa kuwaunganisha wajasiriamali na wateja, wanunuzi, taasisi za fedha, wawekezaji pamoja na wadau wa uendelezaji wa biashara. Mwaka huu maonyesho yanatarajiwa kuwavutia zaidi ya wageni 15,000 na waonyeshaji zaidi ya 300 kutoka sekta mbalimbali zikiwemo kilimo, uvuvi, utalii, ubunifu, viwanda, usindikaji wa vyakula na uchumi wa ubunifu.
Kwa upande wa Stanbic, ushirikiano huu unaakisi mtazamo mpana wa mahitaji halisi ya biashara ili ziweze kufanikiwa. Upatikanaji wa mitaji bado ni jambo la muhimu, lakini ukuaji endelevu pia unategemea uwezo imara wa kuendesha biashara, usimamizi mzuri wa fedha, utayari wa kidijitali, upatikanaji wa masoko, ushauri elekezi pamoja na mitandao sahihi ya kibiashara.

Fredrick Max, Mkuu wa Idara ya Biashara Stanbic Bank, amesema makubaliano haya yanaipa Benki na ZEEA jukwaa muhimu la kuwasaidia wajasiriamali wengi zaidi kugeuza ndoto zao kuwa biashara zenye tija na ushindani. “Zanzibar haikosi wajasiriamali, mawazo, wala dhamira. Fursa iliyopo sasa ni kuzisaidia biashara nyingi zaidi kuugeuza uwezo huo kuwa ukuaji wa kweli. Jambo hilo linahitaji mitaji, lakini pia linahitaji maarifa, mifumo imara ya biashara, uwezo wa kidijitali, masoko na mahusiano. Ushirikiano wetu na ZEEA unaviunganisha vipengele hivi vyote ili wajasiriamali wengi zaidi waweze kujenga biashara zilizo tayari kukua.”

Makubaliano haya pia yatafungua fursa kwa wajasiriamali wanaokidhi vigezo kuunganishwa na programu za Stanbic za uendelezaji wa biashara, ikiwemo Stanbic Biashara Incubator pale inapohusika. Programu hiyo huwapa wajasiriamali msaada wa kivitendo katika kuendeleza biashara, ushauri elekezi, nyenzo na mitandao inayolenga kuimarisha uwezo wa biashara na utayari wa kukua.Katika kipindi chote cha Fahari ya Zanzibar, timu ya Stanbic Biashara Incubator itakuwepo katika viwanja vya maonyesho ikiwahudumia wajasiriamali na kutoa msaada wa kivitendo kwa wafanyabiashara. Timu nyingine za Stanbic pia zitakutana na wafanyabiashara kuzungumzia suluhisho za biashara ya kimataifa, biashara ya kilimo, miamala ya kidijitali pamoja na mikopo ya magari na mitambo.
Stanbic imetoa udhamini wa Shilingi milioni 200 kwa Maonyesho ya Fahari ya Zanzibar 2026 kama Mdhamini wa Ngazi ya Platinamu. Benki inauona uwekezaji huu kama sehemu ya dhamira pana kwa biashara na wajasiriamali watakaoiongoza Zanzibar katika hatua yake ijayo ya ukuaji wa kiuchumi. “Udhamini wetu wa Shilingi milioni 200 si jambo la udhamini pekee. Ni ishara ya imani tuliyo nayo kwa wajasiriamali wa Zanzibar, bidhaa zao na uwezo wa kiuchumi wa visiwa hivi,” amesema Max.

Ushirikiano huu unakuja mwaka mmoja tangu Stanbic ifungue huduma zake Zanzibar, jambo linaloashiria hatua mpya kutoka kuwepo tu na kuelekea kujenga mahusiano ya kina na wananchi na biashara zinazoendesha uchumi wa visiwa.

“Mwaka mmoja tangu tuanze safari yetu hapa, tuko wazi kuhusu nafasi tunayotaka kuichukua. Zanzibar ni nyumbani kwetu, na tunaendelea kuchochea ukuaji wake. Kuiita Zanzibar nyumbani maana yake ni kuwekeza kwa watu wake, biashara zake na uwezo wake wa kiuchumi wa muda mrefu. Tunataka kuzisaidia biashara ziwe imara hapa nyumbani, na kuziunganisha zile zenye dhamira na uwezo na fursa zilizopo Tanzania, Afrika na masoko ya kimataifa,” ameongeza Max.

Juma Burhan Mohamed, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA), amesema ushirikiano huu utaimarisha juhudi za kuwaunganisha wajasiriamali na msaada wanaouhitaji ili kujenga biashara endelevu. “Uwezeshaji wa kiuchumi unahitaji ushirikiano unaowapa wajasiriamali njia za kivitendo za kukua. Kupitia ushirikiano huu, ZEEA na Stanbic zitaunganisha uendelezaji wa biashara, uwezo wa kifedha, upatikanaji wa huduma stahiki za kifedha pamoja na uunganishaji na masoko ili kuwasaidia wajasiriamali wa Unguja na Pemba. Lengo letu ni kutengeneza fursa zinazozaa biashara imara na thamani ya kiuchumi ya kudumu kwa Zanzibar.”

Chini ya Hati hii ya Makubaliano, Stanbic na ZEEA zitaandaa programu mbalimbali zitakazokubaliwa zenye kuunga mkono ujasiriamali, uendelezaji wa biashara ndogo na za kati, upatikanaji wa huduma za kifedha kwa wote, upatikanaji wa mitaji, urasimishaji wa biashara na uunganishaji na masoko. Ushirikiano huu pia utafungua fursa za makongamano ya kibiashara, maonyesho, mafunzo ya kujenga uwezo pamoja na mipango mingine ya uendelezaji wa biashara.

Mafanikio ya ushirikiano huu hatimaye hayatapimwa kwa makubaliano yaliyosainiwa katika Fahari ya Zanzibar pekee. Thamani yake itaonekana katika wajasiriamali imara zaidi, biashara nyingi zaidi zilizo tayari kupata mikopo, bidhaa nyingi zaidi za Zanzibar kufika sokoni, na biashara nyingi zaidi zinazotengeneza ajira na kuchangia ukuaji endelevu wa uchumi wa visiwa hivi.