

Na Mwandishi Wetu, Dodoma.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Christian Makonda, ametangaza kutoutambua mchakato wa kubadilisha jezi za timu za taifa, akisema umefanyika bila kuishirikisha Wizara licha ya maelekezo aliyoyatoa Februari 2026.
Sambamba na hatua hiyo, Waziri Makonda ameagiza kuundwa kwa kamati maalumu itakayochunguza mikataba ya wazabuni wa jezi hizo, manufaa yake kwa timu za taifa pamoja na mapato yanayotokana na mauzo yake.
Uamuzi huo umetangazwa siku mbili baada ya Waziri Makonda kukataa hadharani jezi mpya zilizoonekana zikivaliwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, akisema hazikuwa na ubora unaoendana na hadhi ya Taifa Stars.
“Hii siyo jezi ya Taifa Stars. Taifa Stars kwa ubora wake hatuwezi kuwa na jezi za kiwango cha chini hivi. Acheni kutumia picha za Naibu wangu huku ofisi yangu haina taarifa. Tuheshimiane,” alisema Waziri Makonda kupitia mitandao ya kijamii.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara leo, Septemba 18, 2026, uchunguzi huo unalenga kubaini iwapo mikataba iliyopo inanufaisha timu za taifa kwa kiwango kinacholingana na fedha nyingi zinazotolewa na Serikali kugharamia timu hizo.
Wizara imeeleza kuwa Februari 2026, Waziri Makonda alitoa maelekezo ya kuboresha jezi za timu za taifa ili ziakisi utambulisho wa Tanzania na kuzalisha manufaa mapana kwa nchi.
Hatua hiyo imeelezwa kuwa muhimu kutokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika maandalizi ya timu za taifa zinazoshiriki mashindano ya kimataifa, pamoja na Tanzania kuwa mwenyeji mwenza wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027).
Kamati hiyo pia itachunguza mapato yanayotokana na mauzo ya jezi na mchango wake katika kugharamia uendeshaji wa timu za taifa.

Dar es Salaam-Tanzania, 17 Septemba 2026: Je, umekwama katika ufanyaji wa kazi ambayo unajua kabisa hiyo siyo kwa ajili yako, na umewahi kujiuliza kama kitu ambacho una uwezo nacho ni kile ambacho unakifanya kila siku ukiwa nyumbani, njiani au kwa ajili ya kujifurahisha tu, kinaweza kuwa zaidi ya burudani?
Serengeti Lite, kinywaji pendwa cha Kampuni ya vinywaji ya Serengeti, kwa kushirikiana na KUNTA Africa, wanataka kupata jibu la swali hilo, kwa kutangaza rasmi ujio wa awamu nyingine ya Nyota Bigi msimu wa pili, ambayo inalenga kusaka nyota mkubwa ajaye wa Tanzania, katika mikoa ya Dar es salaam, Mwanza, Arusha na Dodoma. Usaili utaanza jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 3 Oktoba, tarehe 10 safari itaendelea katika mkoa wa Mwanza, Arusha tarehe 17, na Oktoba 24 itakuwa jijini Dodoma.
Msimu wa pili wa Nyota Bigi unatafuta waimbaji, wacheza mziki, waigizaji, wachekeshaji, wabunifu, wana mitindo, na vipaji vingine vya ubunifu ambavyo Tanzania bado haijavivumbua. Mpango huu ni sehemu ya Kampeni ya Serengeti Lite ya “Lite your Imagination” inayolenga kuwahamasisha vijana kuchukulia ubunifu wao kwa uzito, kujieleza na kuona kipaji chao kinaweza kuwafikisha wapi.

Usajili tayari umefunguliwa kupitia msimbo wa QR wa Nyota Bigi, tovuti ya Nyota Bigi, WhatsApp au simu. Waombaji wanapaswa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 35, kuwa na kitambulisho halali na kuwasilisha video fupi inayoonyesha kipaji chao. Usaili utafanyika ana kwa ana na mtandaoni, hivyo kutoa njia mbalimbali kwa wenye vipaji kujitokeza.
Kwa watakaofanikiwa kuvuka hatua hiyo, Nyota Bigi inatoa fursa ya kuingia katika tasnia pana ya ubunifu, huku nafasi zikiongezeka zaidi ya mashindano yenyewe. Washiriki wanaweza kupata fursa za kuunganishwa na maeneo mbalimbali ya masoko kupitia mitandao ya kijamii, uanamitindo, burudani, usimamizi wa vipaji na studio za kurekodi, na hivyo kupata nafasi yakufanikiwa zaidi.
Kwa Serengeti Lite, Nyota Bigi inaweka “Lite Your Imagination” katika vitendo kwa kuwapa vijana nafasi ya kutoka kwenye kufikiria tu kile wanachoweza kufanya na kuanza kukiweka wazi kupitia vipaji vyao. Jukwaa hili ni sehemu ya mwendelezo wa Serengeti Lite katika kukuza ubunifu wa vijana nchini Tanzania.







































.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)



