TRENDING NOW







Na Mwandishi Wetu.

JAMII ya Wandondi na Wandwewe, imetoa mwito wa kitaifa na kimataifa kwa watu wote wenye nia njema kuungana katika Dua Maalum kwa ajili ya Amani, Umoja, Maridhiano, Mshikamano na Ulinzi wa Maisha ya Binadamu.

Dua hiyo ni mwito wa pamoja unaolenga kuwakutanisha watu wa imani, mila, tamaduni na mitazamo mbalimbali katika kusimama kwa pamoja kutetea amani, utu, uhai, mshikamano na heshima kwa mwanadamu, bila kujali tofauti za dini, kabila, rangi, taifa, utamaduni, itikadi au hali ya kijamii.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Chifu Felix G. L. Mfunda, kwa niaba ya jamii ya Wandondi na Wandwewe amesema dua hiyo itafanyika  Agosti 12, 2026,  ambapo Misa Maalumu ya Kikatoliki itafanyika katika Kanisa Katoliki, Kigango cha Mhangazi, Parokia ya Kitanda, Namtumbo, Ruvuma. huku akitoa  mwito wa amani na maridhiano.

Aidha, kuanzia jioni ya Agosti 13 hadi mchana wa Agosti 14, 2026, kutafanyika dua, na shughuli za jadi zitakazoambatana na ngoma na sanaa mbalimbali za asili za Wandwele na Wandondi.

Jamii mbalimbali za Mkoa wa Ruvuma, zikiwemo Makumbo, Lizombe na Makiwa, zinatarajiwa kushiriki katika shughuli hizo zinazolenga kuenzi urithi wa tamaduni, kuimarisha undugu na mshikamano, pamoja na kukuza amani kati ya jamii.

Mfululizo huo utakamilishwa Agosti 16, 2026, kwa Dua Maalumu ya Kiislamu itakayofanyika jioni kwa ajili ya kuiombea Tanzania, Afrika na dunia nzima.
Ambapo  amesema Dunia ya leo inakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo migogoro, vita, chuki, migawanyiko ya kijamii, changamoto za kiuchumi, ukosefu wa usawa na athari za mabadiliko ya tabianchi.

“Katika mazingira haya, tunapaswa kutambua kwamba amani si wajibu wa Serikali pekee; ni wajibu wa kila mwanadamu.Tunatoa mwito kwa viongozi wa kitaifa na kimataifa, viongozi wa dini, viongozi wa kimila, wasomi, vijana, wanawake, mashirika ya kiraia na wananchi wote kutumia nafasi zao kujenga madaraja ya maelewano badala ya kuta za migawanyiko.

“Tunasisitiza umuhimu wa mazungumzo, kusikilizana, kusameheana, kuheshimiana na kutafuta suluhu za amani katika kila tofauti inayojitokeza.”

Aidha amesema ulinzi wa maisha ni wajibu wa pamoja akifafanua maisha ya mwanadamu ni tunu kubwa na hayapaswi kuwekwa rehani kwa sababu ya tofauti za kisiasa, kidini, kikabila, kiuchumi, kijamii au kiitikadi.

Ameongeza kwa msingi huo, wanatoa mwito wa kuheshimiwa kwa utu wa binadamu, haki ya kuishi, usalama wa raia na ulinzi wa watoto, wanawake, wazee na makundi yote yaliyo katika mazingira hatarishi.

“Tunasisitiza tofauti zetu zisigeuke kuwa sababu ya kupoteza maisha ya watu.Kila jamii ina wajibu wa kulinda maisha na kujenga mazingira ambayo kila mwanadamu anaweza kuishi kwa usalama.

Pia amesema kuhusu amani, afya na ulinzi wa mazingira ni kwamba amani ya kweli haiwezi kutenganishwa na afya ya jamii, usalama wa chakula, maji safi, mazingira salama na matumizi endelevu ya rasilimali za asili.

“Uharibifu wa mazingira, ukataji wa misitu, uharibifu wa vyanzo vya maji, upotevu wa bayoanuai na athari za mabadiliko ya tabianchi vinaweza kuongeza changamoto za kijamii na kiuchumi na kuhatarisha maisha ya watu.

“Kwa hiyo, tunatoa mwito wa kuunganisha juhudi za amani, afya, mazingira na maendeleo endelevu kwa ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Akieleza zaidi amesema katika dua kwa Watanzania ,Afrika na Dunia amefafanua Tanzania iendelee kuwa taifa la amani, umoja, mshikamano na utulivu na kwa Afrika ipate amani na utulivu wa kudumu.

Pia migogoro na vita duniani zipungue na hatimaye kumalizika na kuongeza viongozi wapate hekima, busara, uadilifu na moyo wa kuhudumia watu.Vijana wapate fursa za elimu, ajira, ubunifu, ujasiriamali na maendeleo.

Kwa watoto walindwe dhidi ya ukatili, unyanyasaji na mazingira yanayohatarisha maisha yao. Wanawake, wazee na makundi yaliyo katika mazingira magumu walindwe na kuheshimiwa.Wagonjwa na wote wanaokabiliwa na changamoto mbalimbali wapate faraja, matumaini na huduma stahiki na mazingira.

Kuhusu ujumbe kwa Watanzania amesema wanawakumbusha Umoja wetu ni nguvu yetu, amani yetu ni utajiri wetu, na maisha ya kila Mtanzania ni sehemu ya thamani ya Taifa letu.

“Tunapaswa kukataa chuki, uchochezi, ubaguzi, vurugu na lugha zinazogawa jamii. Badala yake, tujenge utamaduni wa kusikilizana, kuheshimiana, kusameheana, kusaidiana na kutatua tofauti zetu kwa njia za amani.

“Tanzania yenye amani na mshikamano ni msingi muhimu wa maendeleo ya watu wake na mchango mkubwa kwa amani ya Afrika na dunia.”


Dar es Salaam, Tanzania: Afrika inapaswa kutumia zaidi mitaji yake ya ndani, kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kukuza masoko ya fedha ya ndani ili kuziba pengo la ufadhili wa miundombinu na kuchochea ukuaji wa uchumi wa muda mrefu, Benki ya Stanbic Tanzania imesema.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wanahisa wa Africa50 na Jukwaa la Miundombinu la Afrika (Africa Infrastructure Forum), lililofanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam, likiwakutanisha viongozi wa kisiasa, wataalamu wa masuala ya fedha na maendeleo kujadili namna taasisi za Afrika zinavyoweza kushirikiana kufadhili maendeleo ya bara, wakati ambapo uwekezaji wa kimataifa unazidi kuwa wa kuchagua.

Akizungumza katika kikao cha mjadala kilichokuwa na mada “Pace Setters: African-Designed, African-Led” (Waongoza Njia: Yaliyobuniwa na Kuongozwa na Waafrika), Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania, Manzi Rwegasira, alisema Afrika tayari ina taasisi imara za kifedha, lakini kinachohitajika sasa ni kuongeza uwezo wa taasisi hizo ili kukidhi mahitaji makubwa na yanayoongezeka ya miundombinu barani.

“Majibu yote mazuri yatatolewa, lakini nadhani yote yanaishia kwenye suala la ukubwa. Tunahitaji kufikiria namna ya kuongeza kiwango cha kile ambacho tayari tunacho katika bara hili,” alisema Rwegasira.

Akielezea mchango wa taasisi kama Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Africa50, Rwegasira alisema taasisi hizo pekee haziwezi kugharamia mahitaji yote ya miundombinu ya Afrika.

Alisema Afrika inapaswa kuongeza uhamasishaji wa rasilimali za ndani, hususan kupitia masoko imara na yenye kina zaidi ya mitaji ya ndani, ambayo yanaweza kusaidia upatikanaji wa fedha kwa ajili ya uwekezaji wa muda mrefu.
“Tunapaswa kutumia vizuri zaidi masoko yetu ya ndani ya hati fungani za serikali. Bado ni madogo na hayana kina cha kutosha. Tunahitaji kuyakuza,” alisema.

Rwegasira pia alitaja ushirikiano wa kikanda kuwa nguzo muhimu katika kufungua vyanzo vikubwa zaidi vya mitaji, akisema nchi za Afrika zinapaswa kuacha kufanya kazi kwa kujitenga na badala yake kutumia nguvu ya pamoja ya rasilimali zilizopo barani.

“Labda ushirikiano wa kikanda ndio mahali tunapoweza kuanzia. Tunahitaji kufanya kazi pamoja kwa ushirikiano ili kutumia mitaji tuliyonayo,” alisema.

Aliongeza kuwa mifumo bunifu ya ufadhili, ikiwemo sekuritizasheni (securitisation) na urejelezaji wa mali za miundombinu (infrastructure asset recycling), inaweza kusaidia serikali kupata uwekezaji wa ziada bila kutegemea pekee vyanzo vipya vya mitaji.

“Securitisation inakuruhusu kutumia tena mtaji uleule tulionao. Ikiwa tunaweza kurejeleza mali za miundombinu, tunaweza kutumia kile ambacho tayari kimejengwa kufadhili miundombinu mipya,” alisema.

Mijadala hiyo iliakisi lengo pana la jukwaa hilo la kuendeleza mfumo wa ufadhili unaoongozwa na Waafrika kupitia **New African Financial Architecture for Development (NAFAD)**, unaolenga kuunganisha nguvu za benki za Afrika, wawekezaji wa kitaasisi, kampuni za bima, taasisi za fedha za maendeleo na serikali katika kufadhili miradi ya miundombinu kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza kando ya mkutano huo, Mkuu wa Kitengo cha Corporate and Investment Banking wa Stanbic Bank Tanzania, Ester Manase, alisema jukwaa hilo limeonesha kuwa ushirikiano ni msingi muhimu katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya miundombinu barani Afrika.
“Mkutano huu umekuwa na manufaa makubwa kwetu kama benki kwa sababu umewakutanisha wadau muhimu ambao wamejikita katika kusaidia maendeleo ya miundombinu barani Afrika,” alisema Manase.

Alisema miundombinu ni kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi kwa kuwa hurahisisha usafirishaji wa mazao ya kilimo na bidhaa nyingine, kuwezesha biashara ya kimataifa na kuchangia katika maendeleo ya uchumi kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Manase, somo kubwa zaidi kutoka katika mkutano huo wa siku mbili ni umuhimu wa ushirikiano kati ya benki za biashara, taasisi za fedha za maendeleo, kampuni za bima, serikali na wawekezaji binafsi, kwa kuwa hakuna taasisi moja inayoweza kugharamia mahitaji ya muda mrefu ya miundombinu ya Afrika pekee.

“Jambo kubwa nililojifunza ni umuhimu wa ushirikiano. Kila mdau ana nafasi muhimu ya kutekeleza, lakini hakuna mmoja wetu anayeweza kufikia malengo haya peke yake,” alisema.

Manase alieleza kuwa ingawa benki za biashara zina nafasi muhimu katika ufadhili wa miundombinu, miradi hiyo inahitaji mitaji ya muda mrefu na yenye uvumilivu, ambayo inaweza kupatikana kupitia ushirikiano na taasisi za fedha za maendeleo pamoja na wawekezaji wa kitaasisi.

“Benki za biashara zinaweza kusaidia ufadhili wa miundombinu kwa kiwango fulani. Kwa kuwa hii ni uwekezaji wa muda mrefu, tunahitaji taasisi za fedha za maendeleo, kampuni za bima, pamoja na sekta ya umma na binafsi kufanya kazi kwa pamoja,” alisema.

Mtendaji huyo pia alisema Tanzania iko katika nafasi nzuri kimkakati ya kuwa lango kuu la usafirishaji na biashara kwa Afrika Mashariki, akitaja uwekezaji unaoendelea katika bandari, reli ya Standard Gauge Railway (SGR) na miundombinu ya barabara.

“Tanzania iko katika eneo la kimkakati sana. Tuna nchi jirani nane, ambapo sita kati ya hizo hazina bandari. Hii inatupa fursa ya kipekee ya kuwa kitovu cha ukanda huu,” alisema.

Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, alisema ufadhili wa miundombinu unapaswa hatimaye kuboresha maisha ya wananchi na hivyo kwenda sambamba na uwekezaji katika rasilimali watu.

Dkt. Kikwete alisema ongezeko la idadi ya vijana barani Afrika linaweza kuwa faida kubwa zaidi ya kiuchumi kwa bara hilo ikiwa serikali zitawekeza katika elimu bora, ukuzaji wa ujuzi na fursa za ajira.

Alisisitiza kuwa barabara, reli na miradi ya nishati haipaswi kuonekana kama mafanikio ya maendeleo yenyewe, bali kama nyenzo za kuongeza uzalishaji, kukuza biashara na kufikia ustawi wa pamoja.

Dar es Salaam-Tanzania, 07th August, 2026: As the International Beer Day is being marked today, Serengeti Breweries Limited (SBL) is marking it uniquely demonstrating the world-class quality of its products. This follows the receiving of Gold Quality Awards – 2026 from the internationally renowned Monde Selection for three of Serengeti Breweries’ brands: Serengeti Lite, Serengeti Lager and Serengeti Lemon.

The Gold Quality Awards, by the Monde Selection, are presented to products that meet the highest international quality standards following a rigorous evaluation by an independent panel of international experts. Products are assessed against a range of criteria, including overall quality, taste, appearance, innovation, consumer information and user experience, to ensure they meet globally recognised benchmarks of excellence.

Founded in 1961 in Brussels, Belgium, Monde Selection is an independent international quality institute specialising in the evaluation of consumer products. For more than 65 years, the institute has assessed thousands of products across various categories, including food, beer, spirits, health and dietary products, and cosmetics. Each year, evaluations are conducted by more than 80 international experts, with products from approximately 150 countries having been submitted for assessment over the years.

This recognition reflects Serengeti Breweries Limited's continued commitment to producing world-class beverages through sustained investment in advanced brewing technologies, robust quality assurance systems and innovation that places consumers at the heart of everything the company does.

Commenting on the achievement, Joseph Cheloti, Supply Chain Director at Serengeti Breweries Limited, said the awards are a testament to the company's unwavering commitment to quality across its product portfolio.

"Receiving the Gold Quality Awards from Monde Selection is a tremendous honour and a strong endorsement that our products meet internationally recognised quality standards. We are proud of this achievement, which reflects the dedication of our people, the quality of the ingredients we use, and the strength of our production processes. Above all, we thank our consumers for their continued trust and loyalty."

He added that the company will continue investing in quality, innovation and product development to ensure consumers in Tanzania and beyond continue to enjoy beverages that meet the highest international standards.

The company’s renowned Spirits Brand, TZEE, also won the Gold Quality Award – 2026. Winning four Gold Quality Awards simultaneously further strengthens Serengeti Breweries Limited's position among leading beverage manufacturers committed to delivering internationally recognised quality while proudly showcasing Tanzania's excellence on the global stage.
Mkurugenzi wa Vodacom Business Nguvu Kamando, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msimu mpya wa msafara wa Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) utakaozinduliwa mnamo mwezi wa kumi ukiambatana na mashindano ya mbio za Vodacom Coastal Classic.
Wadau na Washiriki wa msafara wa mbio za Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) wakipiga makofi kama ishara ya kufurahia ujio wa mashindano ya mbio za Vodacom Coastal Classic.
Mwanzilishi wa Msafara wa Mbio za Twende Butiama, Gabriel Landa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msimu mpya wa msafara wa Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) utakaozinduliwa mnamo mwezi wa kumi.
Wadau wa msafara wa Cycling tour (zamani Twende Butiama) wakisikiliza kwa makini kuhusu msimu mpya wa msafara huo na ujio wa Mashindano ya Vodacom Coastal Classic utakaozinduliwa mnamo mwezi wa kumi mwaka huu.

Na Mwandishi Wetu.

>Msimu mpya kuanza Oktoba ukitanguliwa na Vodacom Coastal Classic

>Ni mashindano ya mbio za baiskeli za km 109 kutoka Dar hadi Bagamoyo

Dar es Salaam, Tanzania, 6 Agosti 2026: Katika hatua muhimu kwa maendeleo ya mchezo wa kuendesha baiskeli nchini Tanzania, Vodacom Tanzania Plc kwa kushirikiana na Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA), leo imetangaza rasmi kubadilishwa kwa jina la msafara wa baiskeli wa Twende Butiama na kuwa Nyerere Cycling Tour, huku pia wakitangaza kuzindua mashindano mapya ya mbio za baiskeli za kilomita 109 za Vodacom Coastal Classic, zinazolenga kuiweka Tanzania kwenye ramani ya kimataifa ya mashindano ya baiskeli.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, msafara huu umekuwa ukienzi urithi wa kudumu wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa kuendeleza fursa sawa kwa wote kupitia uboreshaji wa mazingira ya kujifunzia, ujenzi wa miundombinu ya vyoo, pamoja na kuchangia vifaa vya kuwawezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kila mtoto aweze kupata fursa ya elimu.Hadi sasa, msafara huo umefikia zaidi ya shule 107 na kuboresha maisha ya wanafunzi zaidi ya 75,000 wanaofaidika kupitia ujenzi wa madarasa bora na jumuishi yanayokidhi mahitaji ya wanafunzi wote.

Vodacom Tanzania Foundation ilianza kushirikiana na CHABATA kufadhili msafara huu miaka mine iliyopita, na katika kipindi hicho msafara wa Twende Butiama umekuwa mara nne zaidi, huku ukivutia washiriki kutoka Tanzania, ukanda wa Afrika Mashariki na kimataifa. Msafara wa mwaka huu utafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 14 Oktoba 2026, washiriki wakianzia Bagamoyo hadi Butiama.

Ili kuakisi dhamira kuu ya msafara huu unaoenzi urithi wa Mwalimu Nyerere huku ndani yake wakipanga kuyawezesha kukua ili kuwa mashindano ya kimataifa ya baiskeli, kuanzia mwaka huu msafara huu utajulikana rasmi kama Nyerere Cycling Tour.

Dhamira ya mwaka huu ni moja: kukuza mchezo wa baiskeli na kuiweka Tanzania katika ramani ya kimataifa ya mchezo wa baiskeli. Kwa kushirikiana na CHABATA, Vodacom Tanzania inazindua mashindano makubwa ya baiskeli ya Vodacom Coastal Classic, yakihusisha mbio za kilomita 109 zitakazoshirikisha waendesha baiskeli wa kiume na wa kike.

Mbio hizi zitaanzia Dar es Salaam, kuelekea kaskazini hadi Makurunge mkoani Pwani na kumalizikia katika eneo la kihistoria la Old Boma, Bagamoyo, zikikamilisha safari ya kilomita 109. Kwa mara ya kwanza mashindano haya yatafanyika Jumapili, tarehe 4 Oktoba 2026, siku moja kabla ya kuanza kwa msafara wa baiskeli wa Nyerere Cycling Tour. Baada ya hapo, Vodacom Tanzania itaendesha mashindano haya kila mwaka ifikapo Jumapili ya kwanza ya mwezi Oktoba.

Kwa mara ya kwanza, washiriki zaidi ya 400 kutoka Tanzania na mataifa mbalimbali duniani wanatarajiwa kushiriki katika mbio hizi, "Tunataka kukuza mchezo huu," alisema Nguvu Kamando, Mkurugenzi wa Vodacom Business. "Kila siku tunaona waendesha baiskeli kwenye barabara zetu, aidha wakiwa ni wataalamu au washiriki wa kawaida. Hakuna sababu kwa nini Abella kutoka Mwanza asiweze kushindana hapa Tanzania na kwenye majukwaa ya kimataifa, au Saidi kutoka Shinyanga. Wanachohitaji ni vifaa sahihi na mafunzo sahihi. Vodacom Coastal Classic inalenga kuhamasisha na kuwapa motisha Watanzania wengi zaidi kuingia katika mchezo huu."

Gabriel Landa, Mwanzilishi wa Nyerere Cycling Tour, alisema, "Nyerere Cycling Tour imekuwa zaidi ya msafara wa baiskeli. Ni kuhusu kuendeleza maono ya Mwalimu Nyerere ya heshima na fursa sawa kwa kila Mtanzania. Kubadilisha jina la mashindano haya kwa heshima yake, sambamba na kuanzisha mbio za kiwango cha kimataifa za Vodacom Coastal Classic, ni mwanzo wa safari mpya. Tunajenga jukwaa ambalo vipaji vya Watanzania vinaweza kuibuka na kuvutia waendesha baiskeli kutoka kote duniani kuja kushiriki.

Tarehe Muhimu

Vodacom Coastal Classic (Mashindano ya kilomita 109): Jumapili, 4 Oktoba 2026 — Dar es Salaam hadi Makurunge, zikimalizikia Old Boma, Bagamoyo.

Nyerere Cycling Tour: Tarehe 5–14 Oktoba 2026 — Bagamoyo hadi Butiama.
Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda, ameshangazwa na kiwango cha ubunifu wa teknolojia zinazobuniwa na kuzalishwa na kampuni ya Mati Technologies baada ya kutembelea banda la kampuni hiyo katika Maonesho ya 33 ya Kitaifa ya Kilimo (Nane Nane 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni, jijini Dodoma.

Mhe. Pinda alitembelea banda hilo leo na kupokea maelezo kutoka kwa viongozi na wataalamu wa Mati Technologies kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo katika kubuni na kutengeneza teknolojia zinazolenga kuongeza tija katika sekta ya kilimo na maeneo mengine ya maendeleo.

Katika ziara hiyo, alikagua teknolojia mbalimbali zinazotengenezwa na kampuni hiyo, ikiwemo ndege nyuki zinazotumika kunyunyiza viuatilifu na mbolea mashambani kwa usahihi, haraka na ufanisi mkubwa, pamoja na mifumo mingine ya kisasa ya kiteknolojia inayolenga kuboresha uzalishaji wa kilimo.

Baada ya kushuhudia namna teknolojia hizo zinavyofanya kazi, Mhe. Pinda alisema ameridhishwa na hatua kubwa ya ubunifu iliyofikiwa na wataalamu wa Kitanzania.
“Ni jambo la kujivunia kuona Watanzania wakibuni na kuzalisha teknolojia za kisasa zinazotoa suluhisho kwa changamoto mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta ya kilimo,” alisema.

Alisema maendeleo hayo yanaonesha uwezo mkubwa wa wataalamu wa ndani katika kubuni teknolojia zinazokidhi mahitaji ya nchi na kuchangia kukuza uchumi kupitia sekta ya kilimo na viwanda.
Aidha, aliipongeza Mati Technologies kwa kuwekeza katika utafiti, ubunifu na uzalishaji wa teknolojia za ndani, akisisitiza kuwa juhudi hizo zinapaswa kuungwa mkono ili kuharakisha maendeleo ya taifa na kuongeza ushindani wa bidhaa za Kitanzania katika soko la ndani na kimataifa.

Kwa upande wake, uongozi wa Mati Technologies ulisema kampuni itaendelea kubuni na kuzalisha teknolojia zenye ubora wa hali ya juu zitakazorahisisha shughuli za uzalishaji, kuongeza tija kwa wakulima na kuchochea matumizi ya teknolojia katika sekta mbalimbali za uchumi.
Maonesho ya Nane Nane yameendelea kuwa jukwaa muhimu la kuonesha mafanikio ya sekta za kilimo, mifugo, uvuvi, viwanda na teknolojia, huku yakivutia maelfu ya wananchi, wakulima, wawekezaji, wanafunzi na wataalamu kutoka maeneo mbalimbali nchini.

Kupitia ubunifu wa teknolojia zinazozalishwa hapa nchini, Mati Technologies inaendelea kujijengea sifa kama moja ya kampuni zinazochochea matumizi ya sayansi, teknolojia na utafiti katika kuongeza tija ya uzalishaji na kuchangia maendeleo endelevu ya Tanzania.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta akisaini Kitabu cha wageni, baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akimpigia makofi Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kusaini Kitabu cha wageni katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Waziri wa Nishati wa Tanzania Mhe. Deogratius Ndejembi akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
 Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini Mhe. Dkt. Musenero Masanza wa Uganda akizungumza kwenye mkutano wa Waandishi wa Habari baada ya hafla ya utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda ulioshuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu, jijini Dar es Salaam,
tarehe 06 Agosti, 2026.


Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akutana na Kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu Jijini Dare es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026. Hati hiyo ya Makubaliano imesainiwa kati ya Shirika la Maendeleo la Petroli Tanzania (TPDC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bw. Mussa Makame, Kampuni ya Taifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) chini ya Mkurugenzi Mtendaji Bi. Proscovia Nabbanja pamoja na Kampuni ya Biashara ya Mafuta na Nishati ya Vitol ya Bahrain, chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Tom Baker.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda katika viwanja vya Ikulu, jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiagana na Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuhitimisha ziara rasmi ambapo walishuhudia utiaji saini Hati ya Makubaliano kuhusu mapendekezo ya kuendeleza Tanga kama Kituo cha Nishati cha Kikanda kuwasili katika viwanja vya Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 06 Agosti, 2026.