Articles by "A"
Showing posts with label A. Show all posts

 The upcoming opening of a Plaza Premium Lounge in Dar es Salaam marks long-term commitment to elevating Tanzania’s aviation, tourism, and travel ecosystem.

Dar es Salaam, Tanzania – 5 August, 2026 – Plaza Premium Group (PPG), the global leader in integrated, 360-degree airport hospitality experiences and passenger service solutions, has officially announced its strategic expansion into Tanzania ahead of its upcoming launch of the country’s first Plaza Premium Lounge at Julius Nyerere International Airport (JNIA), Terminal 3 in Dar es Salaam.

To mark this milestone, PPG hosted an executive stakeholder engagement in Dar es Salaam, bringing together key stakeholders across Tanzania's aviation, tourism, financial, corporate and government sectors. The session focused on establishing collaborative partnerships to support Tanzania's premium travel infrastructure and passenger experience.
Scheduled to officially open later this month, Plaza Premium Lounge at JNIA Terminal 3 will welcome all travellers with an elevated pre-flight experience that reflects Plaza Premium Group's award-winning global expertise and thoughtfully integrated local hospitality. Guided by the philosophy of Your Destination Before Departure, the lounge will offer elevated dining and beverage experiences, premium lounge facilities, shower suites, a dedicated prayer room, business amenities and personalised service, creating a seamless and memorable start to every traveller’s journey.

"Tanzania represents one of the most promising aviation and tourism markets in East Africa,” said Okan Kufeci, Senior Vice President, Europe, Middle East and Africa (EMEA), adding that “Continued investment in infrastructure, growing international connectivity, and a vibrant tourism sector are creating the right conditions for premium airport hospitality. Today's engagement marks the beginning of a long-term commitment to collaborate with government institutions, airlines, and industry partners to elevate the passenger experience while supporting Tanzania’s broader growth ambitions.

"This expansion directly supports Tanzania's vision to solidify JNIA as a premier regional hub for international business, trade, and tourism. Operating across more than 600 airports in 150 countries and serving over 30 million passengers annually, PPG brings extensive global operational expertise to the market, seamlessly combining international service standards with authentic local elements to create a refined, destination-inspired journey for every traveller.

Mkurugenzi wa Biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania Plc Brigita Shirima (katikati), Mkurugenzi wa Vodacom Business wa kampuni hiyo Nguvu Kamando (kulia), pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa M-Pesa Tulisindo Mlupilo (kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya "Zaidi ya Mtandao" yenye lengo la kuimarisha dhamira ya kuleta fursa na huduma kwa wateja wake ikiwa ni zaidi ya huduma za mawasiliano ila ni suluhisho halisi la maisha ya kila siku kwa jamii. Tukio hilo limefanyika leo tarehe 4 August 2026, Makao makuu ya Vodacom Tanzania Plc, jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Tanzania, Agosti 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imezindua rasmi kampeni yake ya "Zaidi ya Mtandao" (More Than a Network), hatua inayodhihirisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni ya kutoa zaidi ya huduma za mawasiliano kwa kuwezesha fursa kwa watu, biashara na jamii mbalimbali nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo ya mwaka iliyoishia Machi 2026, Vodacom iliendelea kuongoza soko la mawasiliano nchini kwa kuwa na asilimia 32.3 ya wateja wote, sawa na zaidi ya wateja milioni 36.1. Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya fedha ya kampuni kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2026, Vodacom imeongeza uwekezaji wake karibu mara mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita, ambapo uwekezaji ulifikia shilingi bilioni 123.2. Uwekezaji huo, sambamba na maboresho makubwa ya mfumo wa M-Pesa, unaonesha dhamira ya kampuni ya kutekeleza falsafa ya "Zaidi ya Mtandao" kwa kuharakisha ujumuishaji wa kidijitali nchini na kuwezesha Watanzania wengi zaidi kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Kitengo biashara wa Vodacom Tanzania Plc, Brigita Shirima, alisema kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Vodacom ya kuhakikisha teknolojia inaleta thamani halisi na matokeo chanya kwa wateja.

“Zaidi ya Mtandao” ni ahadi yetu kwamba teknolojia na huduma tunazotoa lazima zilete matokeo chanya. Iwe ni kumsaidia mwanafunzi kupata elimu ya kidijitali, kuwezesha familia kuendelea kuwa karibu au kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao, tunalenga kuunda fursa zinazoboresha maisha. Kwa sababu mtandao haupimwi kwa teknolojia pekee, bali kwa thamani na fursa unazozalisha kwa watu, biashara na jamii," alisema Shirima

Akizungumzia mchango wa suluhisho za kidijitali katika kukuza biashara, Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, alisema mabadiliko ya kidijitali si jambo linalohusu mashirika makubwa pekee, bali yanazalisha na kufungua fursa katika sekta mbalimbali za uchumi ndani ya jamii.

“Biashara za leo zinahitaji zaidi ya huduma wa mawasiliano. Zinahitaji suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kubuni, kushindana na kukua. Kupitia Vodacom Business, tunawezesha kampuni, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma salama za mawasiliano, teknolojia ya utunzaji wa kumbukumbu, teknolojia ya vifaa vilivyounganishwa (Internet of Things - IoT) na majukwaa ya kidijitali yanayoongeza ufanisi na kufungua fursa za kiuchumi. Kwetu, ‘Zaidi ya Mtandao’ kunamaanisha kuwa mshirika wa kuaminika wa kidijitali katika safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” alisema Kamando.

 Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa M-Pesa Vodacom Tanzania Plc, Tulisindo Mlupilo, alisema M-Pesa inaendelea kuwa nguzo muhimu ya ujumuishaji wa kifedha kwa kuwawezesha mamilioni ya Watanzania kupata huduma za kifedha kwa urahisi na usalama.

"Mfumo wa M-Pesa unahudumia zaidi ya watumiaji hai milioni 14.1 kila mwezi kupitia huduma zinazowawezesha kuweka akiba kupitia M-KOBA, kupata mikopo kupitia SONGESHA, kuwekeza kupitia M-WEKEZA, kufanya malipo ya biashara kupitia LIPA na kutuma na kupokea fedha kwa urahisi. Maboresho ya mfumo wa M-Pesa yataongeza uwezo wetu wa kutoa huduma za kifedha kwa ufanisi zaidi na kuendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania za kujenga uchumi wa kidijitali. Dhamira ya Vodacom ni kuendelea kutumia teknolojia kama chachu ya ujumuishaji wa kifedha na kuongeza thamani kwa wateja wetu, tukiendelea kutekeleza falsafa ya ‘Zaidi ya Mtandao’." alisema Mlupilo.

Vodacom inaamini kuwa thamani ya mtandao haipimwi kwa wigo wa huduma, kasi au teknolojia pekee, bali kwa fursa na matokeo chanya unayowezesha katika maisha ya watu kila siku.

Kadri Vodacom inavyoendelea kuwekeza katika mtandao wake, kuboresha uzoefu wa wateja na kuendeleza suluhisho bunifu za kidijitali, "Zaidi ya Mtandao" itaendelea kuwa msingi wa dhamira ya kampuni ya kuunda fursa, kuwezesha maendeleo na kuboresha maisha ya Watanzania.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Kampuni ya Puma Energy Tanzania imezindua rasmi mfumo wake mpya wa kidijitali wa PRIS unaowawezesha wateja kujikusanyia pointi wanaponunua mafuta, vilainishi na bidhaa mbalimbali katika vituo vyake vya huduma nchini.

Uzinduzi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam umeelezwa kuwa sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo wa kuboresha huduma kwa wateja na kuimarisha matumizi ya teknolojia ya kidijitali katika sekta ya nishati.

Kupitia mfumo huo, wateja wataweza kupata zawadi mbalimbali ikiwemo bidhaa za matumizi ya nyumbani, chakula pamoja na punguzo la mafuta baada ya kukusanya kiwango maalumu cha pointi kupitia manunuzi yao ya kila siku.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba aliipongeza Puma Energy Tanzania kwa kuendelea kuboresha huduma zake kwa kutumia mifumo ya kidijitali.


Alisema uzinduzi wa PRIS unaendana na jitihada za serikali za kuimarisha matumizi ya teknolojia katika utoaji wa huduma kwa wananchi na kukuza uchumi wa kidijitali nchini.

“Ubunifu kama huu unaongeza thamani kwa wananchi kwa kuwawezesha kunufaika moja kwa moja na manunuzi yao kupitia mfumo wa pointi na zawadi,” alisema Makamba.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Fatma Abdallah alisema mfumo huo umebuniwa kwa lengo la kuwaweka wateja katikati ya huduma zote zinazotolewa na kampuni hiyo.

“PRIS ni sehemu ya dhamira yetu ya kuendelea kutoa suluhisho zenye manufaa kwa Watanzania. Mfumo huu unabadilisha matumizi ya kila siku kuwa zawadi zenye thamani,” alisema Fatma.
 

Aliongeza kuwa mfumo huo pia unaunga mkono ajenda ya taifa ya mageuzi ya kidijitali kupitia Mfumo wa Kimkakati wa Uchumi wa Kidijitali wa mwaka 2024–2034.

Naye Meneja Mauzo wa Puma Energy Tanzania, Sulpis Mmasi alisema programu hiyo imetengenezwa kwa urahisi ili iweze kutumiwa na watu wengi zaidi.
 Alisema wateja wanaweza kupakua programu hiyo, kujisajili kwa kutumia namba ya simu na kuanza kupata pointi mara moja kwa kuonyesha QR Code wanapofanya malipo katika vituo vya Puma.

“Zaidi ya zawadi, mfumo huu unatoa uzoefu wa kisasa unaomwezesha mteja kufuatilia matumizi yake kwa uwazi na urahisi,” alisema Mmasi.
 Kwa mujibu wa kampuni hiyo, mfumo wa PRIS tayari umefanikiwa katika baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Zimbabwe, Malawi na Botswana ambako umeongeza ushiriki wa wateja katika huduma za kampuni hiyo.

Aidha, Mkuu wa Idara ya Sheria na Mahusiano wa Puma Energy Tanzania, Emmanuel G. Bakilana aliwahimiza wananchi kupakua na kutumia programu hiyo ili kunufaika na huduma mbalimbali zinazotolewa.

Puma Energy Tanzania ni ubia kati ya Puma Energy na Serikali ya Tanzania, huku kampuni hiyo ikiwa na vituo 95 vya mafuta, maduka 30 ya huduma pamoja na vituo vitano vya kuhifadhi mafuta nchini.

Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa amesisitiza kwamba bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27 inapaswa kutoa mwelekeo wa Taifa katika utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote.

Mchengerwa amesema hayo Jumapili Mei 03, 2026 wakati akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wizara ya Afya kilichofanyika ukumbi wa Rock City Mall jijini Mwanza.

"Lazima tujiandae kikamilifu kwa utekelezaji wa Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote. Hili si suala la kadi pekee bali lazima kuwe na utayari wa miundombinu, mifumo, dawa na rasilimali watu imara" alisema Mchengerwa.

Mchengerwa alisisitiza kwamba lazima mifumo ya TEHAMA iwe imara, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba uimarishwe huku akiweka mkazo kwa buzalishaji wa ndani kupewa kipaumbele na Wizara ya Afya.

"Lazima mifumo ya manunuzi itoe kipaumbele kwa wazalishaji wa ndani. Katibu Mkuu nakuagiza usimamie hilo, ununuzi kupitia MSD na mifumo yetu ya manunuzi lazima izingatie hilo lakini kwa kuzingatia ubora" ameongeza.

Mchengerwa aliongeza kuwa katika mwaka wa fedha 2025/2026, Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kupiga hatua ikiwemo kuongeza upatikanaji wa dawa muhimu kufikia wastani wa asilimia 73 kwa mwezi Februari, 2026.

"Pia tumeendelea kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kupitia uwekezaji katika vituo vya afya, hospitali za wilaya, vifaa tiba na rasilimali watu. Haya ni mafanikio ya pamoja chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan" alisema Mchengerwa.

Pia alitoa wito kwa kila mtumishi, kuanzia makao makuu hadi hospitali za rufaa, kutoka idara hadi kituo cha afya, kuhakikisha wanatoa huduma kwa weledi na huruma kwa wananchi.

"Hatutavumilia ucheleweshaji wa huduma usio na sababu. Hatutavumilia upendeleo unaodhalilisha haki za mwananchi" alisisitiza Mchengerwa huku akiagiza Katibu Mkuu kufanyia kazi malalamiko ya wagonjwa kukaa muda mrefu bila kupata huduma katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Dkt Seif Shekalaghe alisema kikao hicho kimelenga kujadili na kupitisha mwelekeo wa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2026/27 yenye lengo la kuboresha huduma za afya kwa wananchi pamoja na ustawi wa watumishi.

Naye Katibu wa Baraza hilo, Vivian Joseph ambaye ni Afisa Tawala Mkuu Wizara ya Afya alisema kupitia kikao hicho kitasaidia upatikanaji wa bajeti ambayo ni shirikishi kutekelezwa na watumishi wa wizara hiyo baada ya kupitishwa na bunge.
Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha baraza kuu la wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika jijini Mwanza.
Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kikao cha baraza kuu la wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika jijini Mwanza.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe akizungumza kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo kilicholenga kujadili na kupitisha bajeti ya mwaka 2026/27.
Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe akizungumza kwenye kikao cha baraza la wafanyakazi Wizara ya Afya kilichoketi jijini Mwanza.
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.
Wafanyakazi wa Wizara ya Afya wakifuatilia kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo.
Na Mwandishi Wetu

Manyara. Kampuni ya Mati Super Brands Ltd imeibuka kinara katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa mwaka 2026, baada ya kuonesha ubunifu wa hali ya juu na ushindani uliovutia katika vipengele mbalimbali vya sherehe hizo.

Katika tukio hilo lililofanyika kwa shamrashamra kubwa, kampuni hiyo ilitwaa ushindi wa jumla, ikiibuka bora katika maandamano ya miguu, ubunifu wa magari pamoja na uandaaji wa banda bora, hatua iliyowavutia waamuzi na washiriki wengine.
Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hizo Mei 1, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, aliipongeza Mati Super Brands Ltd kwa ubunifu na kujituma kwake, akisema imeonesha mfano bora wa ushiriki wa sekta binafsi katika kuadhimisha siku hiyo muhimu kwa wafanyakazi.

“Tumeshuhudia ushindani wa hali ya juu mwaka huu, lakini Mati wamejitofautisha kwa ubunifu, mpangilio na ujumbe waliouwasilisha. Hii ni ishara ya kampuni inayojali wafanyakazi na maendeleo ya jamii,” alisema Sendiga.

Kufuatia ushindi huo, kampuni hiyo ilikabidhiwa kombe la ubingwa wa jumla pamoja na cheti cha pongezi, ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuhamasisha ari ya kazi na ubunifu katika maadhimisho ya Mei Mosi.

Kwa niaba ya kampuni, Afisa Rasilimali Watu wa Mati Super Brands Ltd, Doreen Mushi, alipokea tuzo hizo na kueleza kuwa ushindi huo ni matokeo ya mshikamano na jitihada za wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Alisema kampuni itaendelea kuwekeza katika ubunifu na kuboresha mazingira ya kazi ili kuongeza tija na kuchangia maendeleo ya sekta ya kilimo nchini.

“Ushindi huu unatupa motisha ya kufanya zaidi. Tutazidi kubuni na kuboresha shughuli zetu ili kuendana na mahitaji ya soko na dira ya maendeleo ya taifa,” alisema Mushi.

Naye Mwenyekiti wa Makampuni ya Mati, David Mulokozi, alibainisha kuwa kampuni hiyo inaendelea kuwekeza katika sekta ya kilimo kwa kuzingatia mwelekeo wa serikali wa kuimarisha uzalishaji kupitia teknolojia za kisasa.

Alifafanua kuwa kampuni hiyo imeanza kuzalisha vifaa vya kisasa ikiwemo ndege nyuki (drones) za kunyunyizia dawa mashambani, hatua inayolenga kurahisisha kazi kwa wakulima, kupunguza gharama na kuongeza tija katika uzalishaji.

“Tunataka kuona mkulima wa Tanzania anatumia teknolojia za kisasa ili kuongeza uzalishaji na kipato. Hii ndiyo dira yetu kama kampuni,” alisema Mulokozi.

Maadhimisho ya mwaka huu yamebeba kaulimbiu isemayo “Kazi Zenye Staha ni Nguzo Imara kwa Maendeleo Endelevu katika Utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050,” ikisisitiza umuhimu wa ajira bora na mazingira rafiki ya kazi katika kufikia maendeleo ya muda mrefu ya taifa.

Ushindi wa Mati Super Brands Ltd katika maadhimisho hayo umeendelea kudhihirisha nafasi ya sekta binafsi katika kukuza uchumi, kuhamasisha ubunifu na kuunga mkono juhudi za serikali katika kuboresha maisha ya wananchi kupitia ajira na maendeleo ya kilimo.
Na Mwandishi Wetu.

SHIRIKA la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) limetoa limesisitiza kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda urithi wa mila, utamaduni, tiba asili na mazingira kama nguzo muhimu ya maendeleo endelevu ya Taifa.

TRAMEPRO inasisitiza kuwa maeneo ya mila, maarifa ya tiba asili, pamoja na mifumo ya jadi ya uhifadhi wa mazingira ni sehemu muhimu ya utambulisho wa jamii zetu. Taarifa iliyotolewa leo Aprili 17, 2026 kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu

Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO) Boniventura Mwalongo,

amesema kumekuwepo na changamoto za uvamizi wa maeneo ya mila, mabadiliko holela ya matumizi ya ardhi, pamoja na kuongezeka kwa upotoshaji wa dhana ya tiba asili.

“Mwito kwa Wazee na Machifu wa Mila

TRAMEPRO inatoa wito kwa viongozi wa mila kuendelea kusimamia kwa uaminifu maeneo ya jadi, kulinda urithi wa mababu, na kuendeleza maarifa ya tiba asili. Ushirikiano na Serikali na taasisi husika ni muhimu katika kuhakikisha amani na mshikamano wa kijamii unadumishwa.

Wito kwa Jamii kwa Ujumla

“Wananchi wote wanahimizwa kuthamini urithi wa kitamaduni, kuachana na imani potofu zinazokwamisha maendeleo, na kuzingatia sheria na miongozo rasmi. Umoja na uwajibikaji ni msingi wa ustawi wa Taifa.”

Aidha ametoa ombi kwa Serikali na Wadau wa Maendeleo kuviwezesha na kuviimarisha vikundi vinavyoendeleza tiba asili, utamaduni na uhifadhi wa mazingira, Kuimarisha ushirikiano wa tafiti kati ya taasisi za ndani na za kimataifa na Kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria za ardhi na utamaduni

Pia kuchukua hatua dhidi ya vitendo vinavyosababisha migogoro ya kijamii na uvunjifu wa amani.

“Nukuu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Kuhusu Mazingira na Utamaduni

“Tunapaswa kuthamini na kulinda mila zetu njema pamoja na mazingira yetu, kwa sababu hayo ndiyo msingi wa maendeleo endelevu ya Taifa letu.”

“Pia Shirika linamkumbuka kiongozi mashuhuri wa dunia, Benjamin Franklin, aliyezaliwa tarehe 17 Aprili 1706. Alikuwa mfano wa maarifa, ubunifu na maadili mema, akisisitiza umuhimu wa elimu, nidhamu na hekima katika kujenga jamii imara,” amesema Mwalongo,

Aidha amesema TRAMEPRO inawahimiza wananchi wote kushirikiana katika kulinda urithi wa utamaduni, kuendeleza tiba asili kwa misingi ya sayansi na teknolojia, pamoja na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.