The upcoming opening of a Plaza Premium Lounge in Dar es Salaam marks long-term commitment to elevating Tanzania’s aviation, tourism, and travel ecosystem.
"This expansion directly supports Tanzania's vision to solidify JNIA as a premier regional hub for international business, trade, and tourism. Operating across more than 600 airports in 150 countries and serving over 30 million passengers annually, PPG brings extensive global operational expertise to the market, seamlessly combining international service standards with authentic local elements to create a refined, destination-inspired journey for every traveller.
Na Mwandishi Wetu.
Dar es Salaam, Tanzania, Agosti 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imezindua rasmi kampeni yake ya "Zaidi ya Mtandao" (More Than a Network), hatua inayodhihirisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni ya kutoa zaidi ya huduma za mawasiliano kwa kuwezesha fursa kwa watu, biashara na jamii mbalimbali nchini Tanzania.
Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo ya mwaka iliyoishia Machi 2026, Vodacom iliendelea kuongoza soko la mawasiliano nchini kwa kuwa na asilimia 32.3 ya wateja wote, sawa na zaidi ya wateja milioni 36.1. Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya fedha ya kampuni kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2026, Vodacom imeongeza uwekezaji wake karibu mara mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita, ambapo uwekezaji ulifikia shilingi bilioni 123.2. Uwekezaji huo, sambamba na maboresho makubwa ya mfumo wa M-Pesa, unaonesha dhamira ya kampuni ya kutekeleza falsafa ya "Zaidi ya Mtandao" kwa kuharakisha ujumuishaji wa kidijitali nchini na kuwezesha Watanzania wengi zaidi kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Kitengo biashara wa Vodacom Tanzania Plc, Brigita Shirima, alisema kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Vodacom ya kuhakikisha teknolojia inaleta thamani halisi na matokeo chanya kwa wateja.
“Zaidi ya Mtandao” ni ahadi yetu kwamba teknolojia na huduma tunazotoa lazima zilete matokeo chanya. Iwe ni kumsaidia mwanafunzi kupata elimu ya kidijitali, kuwezesha familia kuendelea kuwa karibu au kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao, tunalenga kuunda fursa zinazoboresha maisha. Kwa sababu mtandao haupimwi kwa teknolojia pekee, bali kwa thamani na fursa unazozalisha kwa watu, biashara na jamii," alisema Shirima
Akizungumzia mchango wa suluhisho za kidijitali katika kukuza biashara, Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, alisema mabadiliko ya kidijitali si jambo linalohusu mashirika makubwa pekee, bali yanazalisha na kufungua fursa katika sekta mbalimbali za uchumi ndani ya jamii.
“Biashara za leo zinahitaji zaidi ya huduma wa mawasiliano. Zinahitaji suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kubuni, kushindana na kukua. Kupitia Vodacom Business, tunawezesha kampuni, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma salama za mawasiliano, teknolojia ya utunzaji wa kumbukumbu, teknolojia ya vifaa vilivyounganishwa (Internet of Things - IoT) na majukwaa ya kidijitali yanayoongeza ufanisi na kufungua fursa za kiuchumi. Kwetu, ‘Zaidi ya Mtandao’ kunamaanisha kuwa mshirika wa kuaminika wa kidijitali katika safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” alisema Kamando.
DAR
ES SALAAM, Tanzania – Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania,
Manzi Rwegasira, atajumuika na viongozi wa kimataifa, mawaziri, watunga
sera, wawekezaji, taasisi za fedha za maendeleo pamoja na viongozi wa
biashara katika Mkutano wa Infra for Africa Forum 2026, unaofanyika
jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 5 hadi 6 Agosti 2026.
Mkutano huo, ulioandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Africa50, utawakutanisha wadau muhimu kujadili mbinu bunifu za kuharakisha maendeleo na uwekezaji katika miundombinu barani Afrika, huku Mgeni Rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Tarehe 5 Agosti, Rwegasira atashiriki katika mjadala wa ngazi ya juu wenye mada “Reinvesting for Expansion: Asset Recycling as a Multiplier”, akiwa pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Nishati na Miundombinu Duniani wa Standard Bank Group, Dele Kuti, na viongozi wengine waandamizi. Katika mjadala huo atazungumzia ugharamiaji wa miundombinu, uhamasishaji wa mitaji na ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuharakisha uwekezaji katika miundombinu barani Afrika.
Tarehe 6 Agosti, pia atazungumza katika kikao cha jumla chenye mada “Pace Setters: African-Designed, African-Led”, sambamba na viongozi waandamizi kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Ecobank, ATIDI na Mfuko wa Uwekezaji wa Taifa wa Angola. Kikao hicho kitachambua namna taasisi za fedha za Afrika, wawekezaji wa kitaifa, benki na wadau wa miundombinu wanavyoweza kuhamasisha mitaji ya ndani, kuimarisha mifumo ya kupunguza hatari na kuharakisha ugharamiaji wa miundombinu kupitia suluhu zinazoongozwa na Waafrika.
Stanbic Bank Tanzania inaeleza kuwa maendeleo ya miundombinu yanaendelea kuwa kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi, mtangamano wa kikanda na ustawi wa muda mrefu, huku ikisisitiza dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo endelevu kupitia suluhu bunifu za kifedha na ushirikiano wa kimkakati unaochochea ajenda ya maendeleo ya Tanzania na ukuaji wa Afrika.

Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza (kushoto), akisalimiana na Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), Dkt. Gozibert Kamugisha (kulia), muda mfupi baada ya Benki ya Exim Tanzania na YST kuzindua ushirikiano wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026 jijini Dar es Salaam. Ushirikiano huo unaofikisha mwaka wa sita unaendelea kuwawezesha vijana wa Kitanzania kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kubuni suluhisho za changamoto za jamii. Kwa mwaka huu, miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari imewasilishwa, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya YST yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo kupitia wataalamu wake, Benki ya Exim Tanzania imeshiriki kutoa ulezi na ushauri wa kitaalamu kwa wanafunzi na walimu ili kuboresha tafiti na ubunifu wao. Uzinduzi wa ushirikiano huo umefanyika tarehe 31 Julai 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Benki ya Exim Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) wamezindua rasmi Programu ya YST 2026, wakiahidi kuendelea kuwawezesha vijana wabunifu kupitia sayansi, teknolojia, utafiti na ubunifu.
Uzinduzi huo uliofanyika Julai 31, 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim (Exim Tower), Dar es Salaam, umeadhimisha miaka sita ya ushirikiano kati ya taasisi hizo katika kukuza vipaji vya wanafunzi wa shule za sekondari nchini.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D'Souza, alisema benki hiyo inaamini kuwa uwekezaji kwa vijana ni msingi wa kujenga taifa lenye ushindani na maendeleo endelevu.
Alisema kupitia falsafa ya benki hiyo ya *"Ubunifu ni Maisha"*, Exim imeendelea kuwaunga mkono wanafunzi wenye vipaji vya ubunifu na kuwapa fursa ya kutumia sayansi na utafiti kutatua changamoto zinazozikabili jamii.
Kwa mujibu wa D'Souza, programu ya mwaka huu imeweka rekodi mpya baada ya kupokea miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari katika mikoa yote ya Tanzania. Baada ya tathmini ya kitaalamu, miradi 162 imechaguliwa kuingia hatua inayofuata, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia yatakayofanyika Septemba 17, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Alieleza kuwa wataalamu wa benki hiyo wamekuwa wakishiriki moja kwa moja katika kutembelea shule, kutoa ushauri wa kitaalamu kwa walimu na wanafunzi pamoja na kusaidia kuboresha tafiti na miradi ya ubunifu.
Hata hivyo, Dkt. Kamugisha alisema YST bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa rasilimali fedha na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya vijana wabunifu.
Alisisitiza kuwa maendeleo ya taifa hayawezi kufikiwa bila uwekezaji wa kutosha katika sayansi, teknolojia na ubunifu wa vijana, akibainisha kuwa mataifa yaliyopiga hatua yamefanikiwa kutokana na kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika tafiti na ugunduzi.
Kwa zaidi ya miaka 16, YST imekuwa ikiwajengea uwezo wanafunzi wa shule za sekondari katika utafiti wa kisayansi na ubunifu, huku ushirikiano wake na Benki ya Exim ukiendelea kusaidia vijana kubuni suluhisho katika maeneo mbalimbali ikiwemo akili unde (AI), kilimo, afya, uhifadhi wa mazingira, usalama wa chakula na teknolojia za mawasiliano.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Vodacom Tanzania PLC imezindua rasmi mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yatakayofanyika katika Uwanja wa Gofu wa Lugalo kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kukuza ushirikiano na kufungua fursa mpya kwa wateja, washirika na wadau wa sekta mbalimbali.
Mashindano hayo, yanayoandaliwa kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited kupitia kitengo cha Vodacom Business, yatawakutanisha viongozi wa makampuni, wafanyabiashara, wataalamu wa sekta mbalimbali na wapenzi wa mchezo wa gofu kwa lengo la kujenga mitandao ya biashara na kubadilishana uzoefu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania PLC, Joseph Sayi, alisema kampuni hiyo imeendelea kudhamini mashindano hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo kwa kuwa yanaendana na dhamira ya kuimarisha mahusiano ya muda mrefu na jumuiya ya wafanyabiashara.
Alisema mashindano hayo si ya michezo pekee, bali ni jukwaa linalowakutanisha viongozi wa biashara, wabunifu na watoa maamuzi ili kujadili fursa mpya za uwekezaji na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.
Sayi alisema katika kipindi chote cha mashindano hayo, Vodacom Business itaonesha suluhisho mbalimbali za kidijitali ikiwemo huduma za mawasiliano, usalama wa kidijitali na teknolojia za biashara zinazosaidia taasisi kuongeza ufanisi, kukuza biashara na kuimarisha ushindani.

Mashindano hayo yatashirikisha timu 10 za makampuni zitakazowania taji la Vodacom Corporate Masters 2026, sambamba na maonesho ya biashara, burudani, maonesho ya vitu vya kale na eneo maalumu la watoto, hatua inayolenga kuwafanya washiriki na familia zao kufurahia tukio hilo katika mazingira rafiki.

Dar es Salaam, Tanzania – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameipatia Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL) Tuzo ya Rais ya Walipakodi Bora katika Sekta ya Uzalishaji (Manufacturing), ikiwa ni kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia ulipaji sahihi wa kodi, uzalishaji wa ndani, uwekezaji na uundaji wa ajira.
Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Mlimani City, Dar es Salaam, Jumatano tarehe 1 Julai 2026.
Uamuzi wa Mheshimiwa Rais kuongoza binafsi utoaji wa tuzo hizo kwa mwaka wa pili mfululizo unaonesha umuhimu ambao Serikali inaweka katika kuhimiza ulipaji wa kodi na kutambua mchango wa sekta binafsi katika kufanikisha maendeleo ya nchi.
Kwa TBL, tuzo hii ni uthibitisho wa mchango mpana wa kampuni katika maendeleo ya Tanzania. Mbali na kulipa kodi kwa wakati na kwa usahihi, kampuni inaendelea kuchangia maendeleo kupitia ajira inazozalisha, ushirikiano wake na wakulima, wasambazaji, wafanyabiashara pamoja na jamii mbalimbali zinazozunguka shughuli zake.
Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Breweries Public Limited Company, Michelle Kilpin, alisema kuwa tuzo hiyo ni ishara ya dhamira ya kampuni ya kuendesha biashara kwa uwajibikaji na kuchangia maendeleo ya Taifa.
"Tunajivunia kupokea heshima hii kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kulipa kodi kikamilifu na kwa wakati ni wajibu wetu kama kampuni ya Kitanzania na sehemu ya mchango wetu katika maendeleo ya nchi. Tuzo hii ni ya wafanyakazi wetu, wakulima, wasambazaji, wauzaji, washirika wetu wa biashara na wadau wote katika mnyororo wetu wa thamani. Tutaendelea kuwekeza nchini na kuwa mshirika wa kuaminika katika safari ya maendeleo ya Tanzania," alisema Kilpin.
Kupitia shughuli zake za uzalishaji wa ndani, TBL inaendelea kuzalisha manufaa yanayovuka mipaka ya viwanda vyake kwa kusaidia wakulima, wasafirishaji, wasambazaji, wafanyabiashara wadogo na wa kati pamoja na wadau wengine wa biashara nchini. Aidha, kupitia ununuzi wa mazao ya ndani kama shayiri (barley) na mtama (sorghum), kampuni inachochea maendeleo ya sekta ya kilimo, kuongeza kipato cha wakulima na kuhakikisha thamani kubwa zaidi ya uchumi inabaki nchini.
Mbali na mchango wake wa kiuchumi, TBL inaendelea kuwekeza katika miradi ya uendelevu ikiwemo usimamizi wa rasilimali za maji, kuwawezesha wakulima, ununuzi wenye uwajibikaji, matumizi ya mifumo ya ufungashaji unaorejelezwa pamoja na programu za urejelezaji wa taka, hatua zinazolenga kuhifadhi mazingira na kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali zinazoiwezesha kampuni kuendesha shughuli zake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Kampuni wa TBL, Neema Temba, alisema kuwa biashara yenye uwajibikaji hupimwa kwa kuzingatia utekelezaji wa sheria pamoja na athari chanya inayozalisha kwa jamii.
"Heshima hii inaakisi msingi wa maadili unaotuongoza kila siku. Tunaamini katika kufanya biashara kwa uwazi, kutimiza wajibu wetu wa kisheria na kushirikiana na Taifa ambalo limekuwa makazi ya biashara yetu kwa miongo mingi. Kampuni zinapolipa kodi stahiki, kuwekeza katika maeneo zinayofanyia kazi na kulinda rasilimali zinazowezesha shughuli zao, nchi nzima hunufaika na kusonga mbele," alisema Temba.
Tuzo hii inaongeza orodha ya mafanikio ambayo TBL imeendelea kuyapata katika maeneo ya ulipaji wa kodi, uendelevu wa biashara na uwajibikaji wa kampuni kwa jamii.
Kadiri Tanzania inavyoendelea kutekeleza agenda ya ukuaji wa viwanda na mageuzi ya uchumi, TBL imesisitiza kuwa itaendelea kuwekeza nchini, kushirikiana na jamii pamoja na kuunda thamani ya kudumu kupitia biashara inayozingatia uwajibikaji.











































