Articles by "HABARI ZA BIASHARA"
Showing posts with label HABARI ZA BIASHARA. Show all posts
Dar es Salaam-Tanzania, 07th August, 2026: As the International Beer Day is being marked today, Serengeti Breweries Limited (SBL) is marking it uniquely demonstrating the world-class quality of its products. This follows the receiving of Gold Quality Awards – 2026 from the internationally renowned Monde Selection for three of Serengeti Breweries’ brands: Serengeti Lite, Serengeti Lager and Serengeti Lemon.

The Gold Quality Awards, by the Monde Selection, are presented to products that meet the highest international quality standards following a rigorous evaluation by an independent panel of international experts. Products are assessed against a range of criteria, including overall quality, taste, appearance, innovation, consumer information and user experience, to ensure they meet globally recognised benchmarks of excellence.

Founded in 1961 in Brussels, Belgium, Monde Selection is an independent international quality institute specialising in the evaluation of consumer products. For more than 65 years, the institute has assessed thousands of products across various categories, including food, beer, spirits, health and dietary products, and cosmetics. Each year, evaluations are conducted by more than 80 international experts, with products from approximately 150 countries having been submitted for assessment over the years.

This recognition reflects Serengeti Breweries Limited's continued commitment to producing world-class beverages through sustained investment in advanced brewing technologies, robust quality assurance systems and innovation that places consumers at the heart of everything the company does.

Commenting on the achievement, Joseph Cheloti, Supply Chain Director at Serengeti Breweries Limited, said the awards are a testament to the company's unwavering commitment to quality across its product portfolio.

"Receiving the Gold Quality Awards from Monde Selection is a tremendous honour and a strong endorsement that our products meet internationally recognised quality standards. We are proud of this achievement, which reflects the dedication of our people, the quality of the ingredients we use, and the strength of our production processes. Above all, we thank our consumers for their continued trust and loyalty."

He added that the company will continue investing in quality, innovation and product development to ensure consumers in Tanzania and beyond continue to enjoy beverages that meet the highest international standards.

The company’s renowned Spirits Brand, TZEE, also won the Gold Quality Award – 2026. Winning four Gold Quality Awards simultaneously further strengthens Serengeti Breweries Limited's position among leading beverage manufacturers committed to delivering internationally recognised quality while proudly showcasing Tanzania's excellence on the global stage.
Mkurugenzi wa Vodacom Business Nguvu Kamando, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msimu mpya wa msafara wa Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) utakaozinduliwa mnamo mwezi wa kumi ukiambatana na mashindano ya mbio za Vodacom Coastal Classic.
Wadau na Washiriki wa msafara wa mbio za Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) wakipiga makofi kama ishara ya kufurahia ujio wa mashindano ya mbio za Vodacom Coastal Classic.
Mwanzilishi wa Msafara wa Mbio za Twende Butiama, Gabriel Landa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msimu mpya wa msafara wa Nyerere Cycling Tour (zamani Twende Butiama) utakaozinduliwa mnamo mwezi wa kumi.
Wadau wa msafara wa Cycling tour (zamani Twende Butiama) wakisikiliza kwa makini kuhusu msimu mpya wa msafara huo na ujio wa Mashindano ya Vodacom Coastal Classic utakaozinduliwa mnamo mwezi wa kumi mwaka huu.

Na Mwandishi Wetu.

>Msimu mpya kuanza Oktoba ukitanguliwa na Vodacom Coastal Classic

>Ni mashindano ya mbio za baiskeli za km 109 kutoka Dar hadi Bagamoyo

Dar es Salaam, Tanzania, 6 Agosti 2026: Katika hatua muhimu kwa maendeleo ya mchezo wa kuendesha baiskeli nchini Tanzania, Vodacom Tanzania Plc kwa kushirikiana na Chama cha Baiskeli Tanzania (CHABATA), leo imetangaza rasmi kubadilishwa kwa jina la msafara wa baiskeli wa Twende Butiama na kuwa Nyerere Cycling Tour, huku pia wakitangaza kuzindua mashindano mapya ya mbio za baiskeli za kilomita 109 za Vodacom Coastal Classic, zinazolenga kuiweka Tanzania kwenye ramani ya kimataifa ya mashindano ya baiskeli.

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, msafara huu umekuwa ukienzi urithi wa kudumu wa Mwalimu Julius K. Nyerere kwa kuendeleza fursa sawa kwa wote kupitia uboreshaji wa mazingira ya kujifunzia, ujenzi wa miundombinu ya vyoo, pamoja na kuchangia vifaa vya kuwawezesha wanafunzi wenye mahitaji maalum ili kila mtoto aweze kupata fursa ya elimu.Hadi sasa, msafara huo umefikia zaidi ya shule 107 na kuboresha maisha ya wanafunzi zaidi ya 75,000 wanaofaidika kupitia ujenzi wa madarasa bora na jumuishi yanayokidhi mahitaji ya wanafunzi wote.

Vodacom Tanzania Foundation ilianza kushirikiana na CHABATA kufadhili msafara huu miaka mine iliyopita, na katika kipindi hicho msafara wa Twende Butiama umekuwa mara nne zaidi, huku ukivutia washiriki kutoka Tanzania, ukanda wa Afrika Mashariki na kimataifa. Msafara wa mwaka huu utafanyika kuanzia tarehe 5 hadi 14 Oktoba 2026, washiriki wakianzia Bagamoyo hadi Butiama.

Ili kuakisi dhamira kuu ya msafara huu unaoenzi urithi wa Mwalimu Nyerere huku ndani yake wakipanga kuyawezesha kukua ili kuwa mashindano ya kimataifa ya baiskeli, kuanzia mwaka huu msafara huu utajulikana rasmi kama Nyerere Cycling Tour.

Dhamira ya mwaka huu ni moja: kukuza mchezo wa baiskeli na kuiweka Tanzania katika ramani ya kimataifa ya mchezo wa baiskeli. Kwa kushirikiana na CHABATA, Vodacom Tanzania inazindua mashindano makubwa ya baiskeli ya Vodacom Coastal Classic, yakihusisha mbio za kilomita 109 zitakazoshirikisha waendesha baiskeli wa kiume na wa kike.

Mbio hizi zitaanzia Dar es Salaam, kuelekea kaskazini hadi Makurunge mkoani Pwani na kumalizikia katika eneo la kihistoria la Old Boma, Bagamoyo, zikikamilisha safari ya kilomita 109. Kwa mara ya kwanza mashindano haya yatafanyika Jumapili, tarehe 4 Oktoba 2026, siku moja kabla ya kuanza kwa msafara wa baiskeli wa Nyerere Cycling Tour. Baada ya hapo, Vodacom Tanzania itaendesha mashindano haya kila mwaka ifikapo Jumapili ya kwanza ya mwezi Oktoba.

Kwa mara ya kwanza, washiriki zaidi ya 400 kutoka Tanzania na mataifa mbalimbali duniani wanatarajiwa kushiriki katika mbio hizi, "Tunataka kukuza mchezo huu," alisema Nguvu Kamando, Mkurugenzi wa Vodacom Business. "Kila siku tunaona waendesha baiskeli kwenye barabara zetu, aidha wakiwa ni wataalamu au washiriki wa kawaida. Hakuna sababu kwa nini Abella kutoka Mwanza asiweze kushindana hapa Tanzania na kwenye majukwaa ya kimataifa, au Saidi kutoka Shinyanga. Wanachohitaji ni vifaa sahihi na mafunzo sahihi. Vodacom Coastal Classic inalenga kuhamasisha na kuwapa motisha Watanzania wengi zaidi kuingia katika mchezo huu."

Gabriel Landa, Mwanzilishi wa Nyerere Cycling Tour, alisema, "Nyerere Cycling Tour imekuwa zaidi ya msafara wa baiskeli. Ni kuhusu kuendeleza maono ya Mwalimu Nyerere ya heshima na fursa sawa kwa kila Mtanzania. Kubadilisha jina la mashindano haya kwa heshima yake, sambamba na kuanzisha mbio za kiwango cha kimataifa za Vodacom Coastal Classic, ni mwanzo wa safari mpya. Tunajenga jukwaa ambalo vipaji vya Watanzania vinaweza kuibuka na kuvutia waendesha baiskeli kutoka kote duniani kuja kushiriki.

Tarehe Muhimu

Vodacom Coastal Classic (Mashindano ya kilomita 109): Jumapili, 4 Oktoba 2026 — Dar es Salaam hadi Makurunge, zikimalizikia Old Boma, Bagamoyo.

Nyerere Cycling Tour: Tarehe 5–14 Oktoba 2026 — Bagamoyo hadi Butiama.

 The upcoming opening of a Plaza Premium Lounge in Dar es Salaam marks long-term commitment to elevating Tanzania’s aviation, tourism, and travel ecosystem.

Dar es Salaam, Tanzania – 5 August, 2026 – Plaza Premium Group (PPG), the global leader in integrated, 360-degree airport hospitality experiences and passenger service solutions, has officially announced its strategic expansion into Tanzania ahead of its upcoming launch of the country’s first Plaza Premium Lounge at Julius Nyerere International Airport (JNIA), Terminal 3 in Dar es Salaam.

To mark this milestone, PPG hosted an executive stakeholder engagement in Dar es Salaam, bringing together key stakeholders across Tanzania's aviation, tourism, financial, corporate and government sectors. The session focused on establishing collaborative partnerships to support Tanzania's premium travel infrastructure and passenger experience.
Scheduled to officially open later this month, Plaza Premium Lounge at JNIA Terminal 3 will welcome all travellers with an elevated pre-flight experience that reflects Plaza Premium Group's award-winning global expertise and thoughtfully integrated local hospitality. Guided by the philosophy of Your Destination Before Departure, the lounge will offer elevated dining and beverage experiences, premium lounge facilities, shower suites, a dedicated prayer room, business amenities and personalised service, creating a seamless and memorable start to every traveller’s journey.

"Tanzania represents one of the most promising aviation and tourism markets in East Africa,” said Okan Kufeci, Senior Vice President, Europe, Middle East and Africa (EMEA), adding that “Continued investment in infrastructure, growing international connectivity, and a vibrant tourism sector are creating the right conditions for premium airport hospitality. Today's engagement marks the beginning of a long-term commitment to collaborate with government institutions, airlines, and industry partners to elevate the passenger experience while supporting Tanzania’s broader growth ambitions.

"This expansion directly supports Tanzania's vision to solidify JNIA as a premier regional hub for international business, trade, and tourism. Operating across more than 600 airports in 150 countries and serving over 30 million passengers annually, PPG brings extensive global operational expertise to the market, seamlessly combining international service standards with authentic local elements to create a refined, destination-inspired journey for every traveller.

Mkurugenzi wa Biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania Plc Brigita Shirima (katikati), Mkurugenzi wa Vodacom Business wa kampuni hiyo Nguvu Kamando (kulia), pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa M-Pesa Tulisindo Mlupilo (kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya "Zaidi ya Mtandao" yenye lengo la kuimarisha dhamira ya kuleta fursa na huduma kwa wateja wake ikiwa ni zaidi ya huduma za mawasiliano ila ni suluhisho halisi la maisha ya kila siku kwa jamii. Tukio hilo limefanyika leo tarehe 4 August 2026, Makao makuu ya Vodacom Tanzania Plc, jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Tanzania, Agosti 4, 2026: Vodacom Tanzania Plc leo imezindua rasmi kampeni yake ya "Zaidi ya Mtandao" (More Than a Network), hatua inayodhihirisha dhamira ya muda mrefu ya kampuni ya kutoa zaidi ya huduma za mawasiliano kwa kuwezesha fursa kwa watu, biashara na jamii mbalimbali nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa robo ya mwaka iliyoishia Machi 2026, Vodacom iliendelea kuongoza soko la mawasiliano nchini kwa kuwa na asilimia 32.3 ya wateja wote, sawa na zaidi ya wateja milioni 36.1. Aidha, kwa mujibu wa taarifa ya fedha ya kampuni kwa robo ya mwaka iliyoishia Juni 2026, Vodacom imeongeza uwekezaji wake karibu mara mbili ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka uliopita, ambapo uwekezaji ulifikia shilingi bilioni 123.2. Uwekezaji huo, sambamba na maboresho makubwa ya mfumo wa M-Pesa, unaonesha dhamira ya kampuni ya kutekeleza falsafa ya "Zaidi ya Mtandao" kwa kuharakisha ujumuishaji wa kidijitali nchini na kuwezesha Watanzania wengi zaidi kushiriki kikamilifu katika uchumi wa kidijitali.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Kitengo biashara wa Vodacom Tanzania Plc, Brigita Shirima, alisema kampeni hiyo inaakisi dhamira ya Vodacom ya kuhakikisha teknolojia inaleta thamani halisi na matokeo chanya kwa wateja.

“Zaidi ya Mtandao” ni ahadi yetu kwamba teknolojia na huduma tunazotoa lazima zilete matokeo chanya. Iwe ni kumsaidia mwanafunzi kupata elimu ya kidijitali, kuwezesha familia kuendelea kuwa karibu au kusaidia wajasiriamali kukuza biashara zao, tunalenga kuunda fursa zinazoboresha maisha. Kwa sababu mtandao haupimwi kwa teknolojia pekee, bali kwa thamani na fursa unazozalisha kwa watu, biashara na jamii," alisema Shirima

Akizungumzia mchango wa suluhisho za kidijitali katika kukuza biashara, Mkurugenzi wa Vodacom Business, Nguvu Kamando, alisema mabadiliko ya kidijitali si jambo linalohusu mashirika makubwa pekee, bali yanazalisha na kufungua fursa katika sekta mbalimbali za uchumi ndani ya jamii.

“Biashara za leo zinahitaji zaidi ya huduma wa mawasiliano. Zinahitaji suluhisho za kidijitali zinazowasaidia kubuni, kushindana na kukua. Kupitia Vodacom Business, tunawezesha kampuni, biashara ndogo na za kati pamoja na taasisi mbalimbali kwa huduma salama za mawasiliano, teknolojia ya utunzaji wa kumbukumbu, teknolojia ya vifaa vilivyounganishwa (Internet of Things - IoT) na majukwaa ya kidijitali yanayoongeza ufanisi na kufungua fursa za kiuchumi. Kwetu, ‘Zaidi ya Mtandao’ kunamaanisha kuwa mshirika wa kuaminika wa kidijitali katika safari ya Tanzania kuelekea Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.” alisema Kamando.

 Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa M-Pesa Vodacom Tanzania Plc, Tulisindo Mlupilo, alisema M-Pesa inaendelea kuwa nguzo muhimu ya ujumuishaji wa kifedha kwa kuwawezesha mamilioni ya Watanzania kupata huduma za kifedha kwa urahisi na usalama.

"Mfumo wa M-Pesa unahudumia zaidi ya watumiaji hai milioni 14.1 kila mwezi kupitia huduma zinazowawezesha kuweka akiba kupitia M-KOBA, kupata mikopo kupitia SONGESHA, kuwekeza kupitia M-WEKEZA, kufanya malipo ya biashara kupitia LIPA na kutuma na kupokea fedha kwa urahisi. Maboresho ya mfumo wa M-Pesa yataongeza uwezo wetu wa kutoa huduma za kifedha kwa ufanisi zaidi na kuendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania za kujenga uchumi wa kidijitali. Dhamira ya Vodacom ni kuendelea kutumia teknolojia kama chachu ya ujumuishaji wa kifedha na kuongeza thamani kwa wateja wetu, tukiendelea kutekeleza falsafa ya ‘Zaidi ya Mtandao’." alisema Mlupilo.

Vodacom inaamini kuwa thamani ya mtandao haipimwi kwa wigo wa huduma, kasi au teknolojia pekee, bali kwa fursa na matokeo chanya unayowezesha katika maisha ya watu kila siku.

Kadri Vodacom inavyoendelea kuwekeza katika mtandao wake, kuboresha uzoefu wa wateja na kuendeleza suluhisho bunifu za kidijitali, "Zaidi ya Mtandao" itaendelea kuwa msingi wa dhamira ya kampuni ya kuunda fursa, kuwezesha maendeleo na kuboresha maisha ya Watanzania.

 DAR ES SALAAM, Tanzania – Mkurugenzi Mtendaji wa Stanbic Bank Tanzania, Manzi Rwegasira, atajumuika na viongozi wa kimataifa, mawaziri, watunga sera, wawekezaji, taasisi za fedha za maendeleo pamoja na viongozi wa biashara katika Mkutano wa Infra for Africa Forum 2026, unaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 5 hadi 6 Agosti 2026.

Mkutano huo, ulioandaliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Africa50, utawakutanisha wadau muhimu kujadili mbinu bunifu za kuharakisha maendeleo na uwekezaji katika miundombinu barani Afrika, huku Mgeni Rasmi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tarehe 5 Agosti, Rwegasira atashiriki katika mjadala wa ngazi ya juu wenye mada “Reinvesting for Expansion: Asset Recycling as a Multiplier”, akiwa pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Nishati na Miundombinu Duniani wa Standard Bank Group, Dele Kuti, na viongozi wengine waandamizi. Katika mjadala huo atazungumzia ugharamiaji wa miundombinu, uhamasishaji wa mitaji na ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuharakisha uwekezaji katika miundombinu barani Afrika.

Tarehe 6 Agosti, pia atazungumza katika kikao cha jumla chenye mada “Pace Setters: African-Designed, African-Led”, sambamba na viongozi waandamizi kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Ecobank, ATIDI na Mfuko wa Uwekezaji wa Taifa wa Angola. Kikao hicho kitachambua namna taasisi za fedha za Afrika, wawekezaji wa kitaifa, benki na wadau wa miundombinu wanavyoweza kuhamasisha mitaji ya ndani, kuimarisha mifumo ya kupunguza hatari na kuharakisha ugharamiaji wa miundombinu kupitia suluhu zinazoongozwa na Waafrika.

Stanbic Bank Tanzania inaeleza kuwa maendeleo ya miundombinu yanaendelea kuwa kichocheo muhimu cha ukuaji wa uchumi, mtangamano wa kikanda na ustawi wa muda mrefu, huku ikisisitiza dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo endelevu kupitia suluhu bunifu za kifedha na ushirikiano wa kimkakati unaochochea ajenda ya maendeleo ya Tanzania na ukuaji wa Afrika.

Mtoa huduma wa Vodacom Tanzania Catherine Masanja (kushoto) akimsajilia line ya Lipa mkazi wa Igoma Irene Ernest, kwenye maonesho ya Wakulima katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza, Kampuni hiyo iko katika maonesho ya Nanenane ikiwaelezea wananchi bidhaa na huduma mablimbali inazotoa ikiwamo M-Kulima huduma inayowapa wakulima njia rahisi na salama ya kulipwa mapato yao pindi wanapouza mazao mbalimbali.
Mtoa huduma wa Vodacom Tanzania, akiwaeleza wateja kuhusu Router kwenye maonesho ya Wakulima katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza.
Kampuni ya Vodacom Tanzania inaendelea kuimarisha huduma za kifedha na mawasiliano kwa wananchi kupitia ushiriki wake katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nyamhongolo mkoani Mwanza.

Katika maonesho hayo, watoa huduma wa kampuni hiyo wamekuwa wakitoa elimu na kusajili wananchi kwenye huduma mbalimbali, ikiwemo huduma ya Lipa.

Kupitia huduma ya M-Kulima, Vodacom inalenga kuwapatia wakulima suluhisho rahisi, salama na la uhakika la kupokea malipo yao wanapouza mazao. 

Huduma hii inalenga kuongeza uwazi na ufanisi katika miamala ya kifedha kwa wakulima, huku ikichangia kukuza uchumi wa sekta ya kilimo nchini. Vodacom inaendelea kujitolea kutoa huduma bunifu zitakazowawezesha wananchi, hasa wakulima, kunufaika zaidi na teknolojia ya kidijitali.

Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D’souza (kushoto), akisalimiana na Mwanzilishi Mwenza wa Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST), Dkt. Gozibert Kamugisha (kulia), muda mfupi baada ya Benki ya Exim Tanzania na YST kuzindua ushirikiano wa mwaka 2026 kupitia Programu ya YST 2026 jijini Dar es Salaam. Ushirikiano huo unaofikisha mwaka wa sita unaendelea kuwawezesha vijana wa Kitanzania kutumia sayansi, utafiti na ubunifu kubuni suluhisho za changamoto za jamii. Kwa mwaka huu, miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari imewasilishwa, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia ya YST yatakayofanyika tarehe 17 Septemba 2026 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambapo kupitia wataalamu wake, Benki ya Exim Tanzania imeshiriki kutoa ulezi na ushauri wa kitaalamu kwa wanafunzi na walimu ili kuboresha tafiti na ubunifu wao. Uzinduzi wa ushirikiano huo umefanyika tarehe 31 Julai 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim Tanzania.

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Benki ya Exim Tanzania kwa kushirikiana na Taasisi ya Wanasayansi Chipukizi Tanzania (YST) wamezindua rasmi Programu ya YST 2026, wakiahidi kuendelea kuwawezesha vijana wabunifu kupitia sayansi, teknolojia, utafiti na ubunifu.

Uzinduzi huo uliofanyika Julai 31, 2026 katika Makao Makuu ya Benki ya Exim (Exim Tower), Dar es Salaam, umeadhimisha miaka sita ya ushirikiano kati ya taasisi hizo katika kukuza vipaji vya wanafunzi wa shule za sekondari nchini.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Meneja Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Kauthar D'Souza, alisema benki hiyo inaamini kuwa uwekezaji kwa vijana ni msingi wa kujenga taifa lenye ushindani na maendeleo endelevu.

Alisema kupitia falsafa ya benki hiyo ya *"Ubunifu ni Maisha"*, Exim imeendelea kuwaunga mkono wanafunzi wenye vipaji vya ubunifu na kuwapa fursa ya kutumia sayansi na utafiti kutatua changamoto zinazozikabili jamii.

Kwa mujibu wa D'Souza, programu ya mwaka huu imeweka rekodi mpya baada ya kupokea miradi 1,330 kutoka shule 287 za sekondari katika mikoa yote ya Tanzania. Baada ya tathmini ya kitaalamu, miradi 162 imechaguliwa kuingia hatua inayofuata, huku miradi 45 bora ikitarajiwa kushiriki Maonesho ya Kitaifa ya Sayansi na Teknolojia yatakayofanyika Septemba 17, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Kwa upande wake, Mwanzilishi Mwenza wa YST, Dkt. Gozbert Kamugisha, aliishukuru Benki ya Exim Tanzania kwa kuendelea kuisaidia taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka sita, akisema ushirikiano huo umeongeza zaidi ya udhamini wa kifedha.

Alieleza kuwa wataalamu wa benki hiyo wamekuwa wakishiriki moja kwa moja katika kutembelea shule, kutoa ushauri wa kitaalamu kwa walimu na wanafunzi pamoja na kusaidia kuboresha tafiti na miradi ya ubunifu.

Hata hivyo, Dkt. Kamugisha alisema YST bado inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa rasilimali fedha na uelewa mdogo wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwekeza katika maendeleo ya vijana wabunifu.

Alisisitiza kuwa maendeleo ya taifa hayawezi kufikiwa bila uwekezaji wa kutosha katika sayansi, teknolojia na ubunifu wa vijana, akibainisha kuwa mataifa yaliyopiga hatua yamefanikiwa kutokana na kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika tafiti na ugunduzi.

Kwa zaidi ya miaka 16, YST imekuwa ikiwajengea uwezo wanafunzi wa shule za sekondari katika utafiti wa kisayansi na ubunifu, huku ushirikiano wake na Benki ya Exim ukiendelea kusaidia vijana kubuni suluhisho katika maeneo mbalimbali ikiwemo akili unde (AI), kilimo, afya, uhifadhi wa mazingira, usalama wa chakula na teknolojia za mawasiliano.

Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Upendo Wella (kushoto), na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania, Bi. Fatma Abdalla (kulia), wakipanda na kumwagilia mti katika Shule ya Msingi Usule, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, ikiwa ni sehemu ya shughuli za uwajibikaji kwa jamii zilizotekelezwa na Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania wakati wa hafla ya uzinduzi wa kituo chake cha 100 cha huduma za mafuta nchini, kilichozinduliwa mkoani Tabora tarehe 22 Julai 2026. Kama sehemu ya uzinduzi huo, Kampuni hiyo pia ilikabidhi madawati 100 kwa Shule ya Msingi Usule kwa lengo la kupunguza changamoto ya upungufu wa madawati na kuwawezesha wanafunzi kupata mazingira bora na salama ya kujifunzia, pamoja na kutoa magodoro 100 kwa Kituo cha Kulelea Watoto cha Istiqaama kwa ajili ya kuboresha mazingira ya maisha ya watoto wanaoishi katika kituo hicho.
Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Upendo Wella (katikati), akikata utepe kuzindua rasmi kituo cha 100 cha huduma za mafuta ya rejareja cha Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania nchini, kilichopo eneo la Usule, Mkoa wa Tabora. Kituo hicho ni cha kwanza cha Kampuni hiyo mkoani Tabora na kitawawezesha wakazi wa Tabora na maeneo jirani kupata huduma za mafuta, vilainishi vya Puma, gesi ya kupikia ya PumaGas pamoja na fursa za kujipatia pointi kupitia mpango wa Puma Pris. Uzinduzi huo ni sehemu ya upanuzi wa mtandao wa huduma za mafuta wa Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania unaolenga kuimarisha upatikanaji wa nishati salama na ya uhakika nchini. Hafla hiyo iliyofanyika tarehe 22 Julai 2026 ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Meya wa Manispaa ya Tabora, Mheshimiwa Gulam Dewji (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania, Bi. Fatma Abdalla (wa pili kushoto), Katibu Tawala wa Wilaya ya Tabora, Bi. Asha Churu (wa pili kulia), pamoja na mmiliki wa kituo hicho, Bw. Kishimba Kibera (kulia).
Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Mhe. Upendo Wella (kushoto), akipokea dawati kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania, Bi. Fatma Abdalla (kulia), ikiwa ni sehemu ya madawati 100 yaliyotolewa na Kampuni hiyo kwa Shule ya Msingi Usule, iliyopo Kata ya Mbugani, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora. Msaada huo unaolenga kupunguza changamoto ya upungufu wa madawati na kuwawezesha wanafunzi kupata mazingira bora na salama ya kujifunzia ni sehemu ya shughuli za uwajibikaji kwa jamii zilizotekelezwa na Kampuni ya Nishati ya Puma Tanzania wakati wa uzinduzi wa kituo chake cha 100 cha huduma za mafuta nchini, kilichozinduliwa mkoani Tabora tarehe 22 Julai 2026.

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Nishati ya Puma Tanzania imezindua rasmi kituo chake cha 100 cha huduma za mafuta nchini, huku ikifungua kituo chake cha kwanza mkoani Tabora katika hatua inayolenga kuimarisha upatikanaji wa nishati salama na kuchochea maendeleo ya kiuchumi.

Kituo hicho kilichopo mjini Tabora kilizinduliwa Julai 22, 2026 na Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Upendo Wella, akishirikiana na viongozi wa serikali, wawakilishi wa wananchi, wateja pamoja na menejimenti ya kampuni hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Tanzania, Fatma Abdalla, alisema kufikisha vituo 100 ni ishara ya imani ya kampuni katika uchumi wa Tanzania na dhamira yake ya kuendelea kuwekeza katika miundombinu ya nishati.

Alisema uwekezaji huo utarahisisha upatikanaji wa mafuta ya uhakika, kuimarisha biashara, kuchochea shughuli za usafirishaji na kuongeza fursa za ajira, hususan katika mkoa wa Tabora ambao unaendelea kukua kwa shughuli za kilimo na biashara.

"Kuanzisha kituo chetu cha 100 si tu kupanua mtandao wa huduma, bali ni kuimarisha ushirikiano wetu wa muda mrefu na Tanzania. Tunaamini upatikanaji wa nishati ya uhakika unafungua fursa za maendeleo kwa wananchi na uchumi wa taifa," alisema Abdalla.

Mbali na uwekezaji huo, kampuni hiyo ilitekeleza shughuli mbalimbali za uwajibikaji kwa jamii (CSR), ikitoa magodoro 100 kwa Kituo cha Kulelea Watoto cha Istiqaama, madawati 100 kwa Shule ya Msingi Usule pamoja na kupanda miti 100 kwa kushirikiana na wananchi ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuhifadhi mazingira.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tabora, Upendo Wella, aliipongeza Puma Tanzania kwa kuendelea kuwekeza nchini, akisema hatua hiyo itaongeza ajira, kuimarisha biashara za ndani na kuchangia maendeleo ya mkoa huo.

Alisema uwekezaji wa kampuni hiyo unaonesha imani ya wawekezaji katika mazingira ya biashara nchini na kuwataka wawekezaji wengine kutumia fursa zilizopo mkoani Tabora.

Puma Tanzania ni sehemu ya Kampuni ya Nishati ya Puma inayofanya shughuli zake katika zaidi ya nchi 34 duniani, ikitoa huduma za usambazaji wa mafuta, mafuta ya anga, vilainishi na lami kwa kuzingatia viwango vya usalama, ubora na maendeleo endelevu.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (katikati) akizungumza wakati wa kutangaza udhamini wa Mashindano ya Golf ya Vodacom Corporate Masters 2026, yaliyoandaliwa kwa ushirikiano na Lugalo Golf Club kwa lengo la kuunganisha jumuiya ya wafanyabiashara nchini Tanzania, kuimarisha mahusiano ya kibiashara, kukuza ushirikiano na kuleta fursa zenye tija kwa wateja, washirika wa kibiashara na wadau muhimu nchini. Mashindano hayo yatakayofanyika tarehe 1 Agosti 2026 yanaendelea kuimarisha nafasi ya Vodacom kama mshirika wa kuaminika katika teknolojia na huduma za mawasiliano kwa taasisi na mashirika yanayoendelea kukua katika mazingira ya uchumi wa kidijitali. Uzinduzi huo umefanyika tarehe 16 Julai 2026 jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Katibu wa Corporate Masters, Maryanne Mugo (kushoto) pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Corporate Masters, Ken Mbaya (kulia).

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Vodacom Tanzania PLC imezindua rasmi mashindano ya Vodacom Corporate Masters 2026 yatakayofanyika katika Uwanja wa Gofu wa Lugalo kuanzia Agosti 1, 2026, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano wa kibiashara, kukuza ushirikiano na kufungua fursa mpya kwa wateja, washirika na wadau wa sekta mbalimbali.

Mashindano hayo, yanayoandaliwa kwa kushirikiana na Oakwood Holdings Limited kupitia kitengo cha Vodacom Business, yatawakutanisha viongozi wa makampuni, wafanyabiashara, wataalamu wa sekta mbalimbali na wapenzi wa mchezo wa gofu kwa lengo la kujenga mitandao ya biashara na kubadilishana uzoefu.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania PLC, Joseph Sayi, alisema kampuni hiyo imeendelea kudhamini mashindano hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo kwa kuwa yanaendana na dhamira ya kuimarisha mahusiano ya muda mrefu na jumuiya ya wafanyabiashara.

Alisema mashindano hayo si ya michezo pekee, bali ni jukwaa linalowakutanisha viongozi wa biashara, wabunifu na watoa maamuzi ili kujadili fursa mpya za uwekezaji na kuharakisha safari ya Tanzania kuelekea uchumi wa kidijitali.

Sayi alisema katika kipindi chote cha mashindano hayo, Vodacom Business itaonesha suluhisho mbalimbali za kidijitali ikiwemo huduma za mawasiliano, usalama wa kidijitali na teknolojia za biashara zinazosaidia taasisi kuongeza ufanisi, kukuza biashara na kuimarisha ushindani.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Corporate Masters, Ken Kariuki, alisema mashindano hayo yameendelea kuwa jukwaa muhimu la makampuni kujitangaza, kujenga mitandao ya kibiashara na kuzalisha fursa mpya za biashara huku yakiimarisha ushiriki wa wateja.

Mashindano hayo yatashirikisha timu 10 za makampuni zitakazowania taji la Vodacom Corporate Masters 2026, sambamba na maonesho ya biashara, burudani, maonesho ya vitu vya kale na eneo maalumu la watoto, hatua inayolenga kuwafanya washiriki na familia zao kufurahia tukio hilo katika mazingira rafiki.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Uwezeshaji, Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (kulia) na Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa kampuni hiyo Happiness Shuma (kushoto), wakiwa wameshika tuzo zilizotolewa kwa Vodacom Tanzania kutambua mchango wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA). Maonesho hayo yaliyofanyika Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yaliipa Vodacom Tanzania fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini.
Meneja Masoko wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Caleb Majo (kushoto), akitoa elimu kuhusu huduma zinazotolewa na Vodacom Tanzania wakati wa mahojiano maalumu na Azam Media katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA). Maonesho hayo yaliyofanyika Juni 28 hadi Julai 13, 2026, yaliipa Vodacom Tanzania fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini. Wengine ni Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania Plc, Alex Bitekeye (wa pili kushoto), Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Happiness Shuma (wa pili kulia), na Mtangazaji wa Azam Media, Jafar Mponda (kulia).
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi (aliyekaa katikati), Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga (aliyekaa kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE, Latifa Khamis (aliyekaa kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa kampuni mbalimbali, akiwemo Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa Vodacom Tanzania Plc, Happiness Shuma (aliyevaa tisheti nyekundu), muda mfupi baada ya kufungwa kwa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (SABASABA). Vodacom Tanzania Plc ilitambuliwa kama mshirika muhimu wa maonesho hayo baada ya kupewa tuzo mbili; Tuzo ya Nafasi ya Tatu kwa Mshindi wa Jumla wa Maonesho na Tuzo ya Nafasi ya Pili ya Udhamini, ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika kufanikisha maonesho hayo.
Mkuu wa idara ya Masoko na Uwezeshaji wa Vodacom Tanzania Plc, Joseph Sayi (wa sita kulia), na Mkuu wa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani wa kampuni hiyo Happiness Shuma (wa sita kushoto) wakiwa katika picha ya Pamoja na wafanyakazi wengine wa Vodacom wakiwa wa wameshika tuzo zilizotolewa kwa Vodacom Tanzania kutambua mchango wake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (SABASABA) muda mfupi baada ya kufungwa rasmi kwa maonesho hayo. Kwa siku zote 13 za maonesho hayo Vodacom Tanzania ilishiriki fursa ya kuonyesha namna teknolojia inavyobadilisha maisha, kuwezesha huduma za kidijitali na kuimarisha nafasi yake kama kinara wa huduma za mawasiliano nchini.

Na Mwandishi Wetu

Dar es Salaam. Kampuni ya Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL) imeendelea kuonesha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya jamii na uchumi wa ndani kupitia kampeni yake ya Cheers to Bars, inayotambua mchango mkubwa wa baa katika kuwaleta watu pamoja, kukuza biashara ndogo ndogo na kuimarisha shughuli za kiuchumi nchini.

TBL imesema kuwa baa zimekuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku ya Watanzania, zikitoa nafasi kwa marafiki na majirani kukutana, mashabiki wa soka kushuhudia mechi pamoja na wafanyabiashara wadogo kuendesha shughuli zao. Kampeni hiyo inalenga kuzisherehekea baa kwa mchango wake katika kujenga mshikamano wa kijamii na kuchochea maendeleo ya uchumi.

Mbali na kuwa sehemu za burudani, TBL imeeleza kuwa baa zimeendelea kutoa ajira kwa maelfu ya Watanzania, wakiwemo wamiliki wa baa, wahudumu, wauzaji wa chakula, wasambazaji wa bidhaa, walinzi, wasafishaji pamoja na watoa huduma za usafiri, hali inayochangia kuongeza kipato kwa watu wengi na kuimarisha mzunguko wa fedha katika jamii.

Kampeni ya Cheers to Bars pia imeangazia nafasi ya baa wakati wa matukio makubwa ya michezo, hususan soka, ambapo mashabiki wengi hupendelea kutazama mechi kwa pamoja katika mazingira yanayowapa fursa ya kushirikiana, kushangilia na kujenga kumbukumbu za pamoja.

Hali hiyo ilijidhihirisha katika Baa ya Kitambaa Cheupe jijini Dar es Salaam, ambapo mashabiki walikusanyika kushuhudia mechi ya robo fainali kati ya Hispania na Ubelgiji. Mechi hiyo iligeuka kuwa zaidi ya mchezo wa soka, huku ikiunganisha watu wa kada mbalimbali walioshiriki kushangilia na kufurahia burudani kwa pamoja.
Akizungumza kuhusu kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Ushirika wa TBL, Neema Temba, alisema Cheers to Bars si kampeni inayolenga soka pekee, bali ni jukwaa la kutambua mchango wa baa na watu wanaoziendesha katika maendeleo ya jamii na uchumi wa Tanzania.

"Baa ni sehemu muhimu ya maisha ya kijamii na kiuchumi ya Watanzania. Zinasaidia kujenga maisha ya watu, zinatoa fursa kwa biashara ndogo ndogo na zinatoa nafasi kwa jamii kukutana na kuimarisha mahusiano. Kupitia Cheers to Bars, tunazisherehekea baa hizi pamoja na watu wanaoziendesha, huku tukiwahamasisha watumiaji kufurahia vinywaji kwa kuwajibika," alisema Neema.
Aliongeza kuwa wakati wa mechi kubwa za soka, shughuli za biashara huongezeka kwa kiasi kikubwa katika baa na maeneo yanayozizunguka. Wauzaji wa chakula, wasambazaji wa bidhaa, madereva wa usafiri na watoa huduma wengine wote hunufaika kutokana na ongezeko la wateja, jambo linaloifanya sekta ya ukarimu kuwa kichocheo muhimu cha uchumi wa ndani.

Kwa mujibu wa TBL, mafanikio ya kampeni hiyo yanaonesha kuwa baa za kienyeji zimeendelea kuwa sehemu muhimu zinazochangia maendeleo ya jamii kwa kuunganisha watu kupitia michezo na burudani, huku zikitoa fursa za ajira na biashara kwa makundi mbalimbali.

Kampuni hiyo imewataka Watanzania kuendelea kuunga mkono baa za kienyeji na kushiriki burudani katika mazingira salama kwa kutumia vinywaji kwa uwajibikaji. TBL imeeleza kuwa itaendelea kutekeleza kampeni ya Cheers to Bars kama sehemu ya juhudi zake za kuthamini mchango wa baa katika ukuaji wa uchumi, maendeleo ya jamii na ustawi wa sekta ya ukarimu nchini.

Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akikabidhi Tuzo ya Rais ya Walipakodi Bora katika Sekta ya Uzalishaji kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL), Michelle Kilpin wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Mlimani City, Dar es Salaam, Jumatano tarehe 1 Julai 2026.

Na Mwandishi Wetu.

Dar es Salaam, Tanzania – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameipatia Tanzania Breweries Public Limited Company (TBL) Tuzo ya Rais ya Walipakodi Bora katika Sekta ya Uzalishaji (Manufacturing), ikiwa ni kutambua mchango wa kampuni hiyo katika kukuza uchumi wa Taifa kupitia ulipaji sahihi wa kodi, uzalishaji wa ndani, uwekezaji na uundaji wa ajira.

Tuzo hiyo ilitolewa wakati wa maadhimisho ya miaka 30 ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Mlimani City, Dar es Salaam, Jumatano tarehe 1 Julai 2026.

Uamuzi wa Mheshimiwa Rais kuongoza binafsi utoaji wa tuzo hizo kwa mwaka wa pili mfululizo unaonesha umuhimu ambao Serikali inaweka katika kuhimiza ulipaji wa kodi na kutambua mchango wa sekta binafsi katika kufanikisha maendeleo ya nchi.

Kwa TBL, tuzo hii ni uthibitisho wa mchango mpana wa kampuni katika maendeleo ya Tanzania. Mbali na kulipa kodi kwa wakati na kwa usahihi, kampuni inaendelea kuchangia maendeleo kupitia ajira inazozalisha, ushirikiano wake na wakulima, wasambazaji, wafanyabiashara pamoja na jamii mbalimbali zinazozunguka shughuli zake.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Breweries Public Limited Company, Michelle Kilpin, alisema kuwa tuzo hiyo ni ishara ya dhamira ya kampuni ya kuendesha biashara kwa uwajibikaji na kuchangia maendeleo ya Taifa.

"Tunajivunia kupokea heshima hii kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kulipa kodi kikamilifu na kwa wakati ni wajibu wetu kama kampuni ya Kitanzania na sehemu ya mchango wetu katika maendeleo ya nchi. Tuzo hii ni ya wafanyakazi wetu, wakulima, wasambazaji, wauzaji, washirika wetu wa biashara na wadau wote katika mnyororo wetu wa thamani. Tutaendelea kuwekeza nchini na kuwa mshirika wa kuaminika katika safari ya maendeleo ya Tanzania," alisema Kilpin.

Kupitia shughuli zake za uzalishaji wa ndani, TBL inaendelea kuzalisha manufaa yanayovuka mipaka ya viwanda vyake kwa kusaidia wakulima, wasafirishaji, wasambazaji, wafanyabiashara wadogo na wa kati pamoja na wadau wengine wa biashara nchini. Aidha, kupitia ununuzi wa mazao ya ndani kama shayiri (barley) na mtama (sorghum), kampuni inachochea maendeleo ya sekta ya kilimo, kuongeza kipato cha wakulima na kuhakikisha thamani kubwa zaidi ya uchumi inabaki nchini.

Mbali na mchango wake wa kiuchumi, TBL inaendelea kuwekeza katika miradi ya uendelevu ikiwemo usimamizi wa rasilimali za maji, kuwawezesha wakulima, ununuzi wenye uwajibikaji, matumizi ya mifumo ya ufungashaji unaorejelezwa pamoja na programu za urejelezaji wa taka, hatua zinazolenga kuhifadhi mazingira na kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali zinazoiwezesha kampuni kuendesha shughuli zake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sheria na Masuala ya Kampuni wa TBL, Neema Temba, alisema kuwa biashara yenye uwajibikaji hupimwa kwa kuzingatia utekelezaji wa sheria pamoja na athari chanya inayozalisha kwa jamii.

"Heshima hii inaakisi msingi wa maadili unaotuongoza kila siku. Tunaamini katika kufanya biashara kwa uwazi, kutimiza wajibu wetu wa kisheria na kushirikiana na Taifa ambalo limekuwa makazi ya biashara yetu kwa miongo mingi. Kampuni zinapolipa kodi stahiki, kuwekeza katika maeneo zinayofanyia kazi na kulinda rasilimali zinazowezesha shughuli zao, nchi nzima hunufaika na kusonga mbele," alisema Temba.

Tuzo hii inaongeza orodha ya mafanikio ambayo TBL imeendelea kuyapata katika maeneo ya ulipaji wa kodi, uendelevu wa biashara na uwajibikaji wa kampuni kwa jamii.

Kadiri Tanzania inavyoendelea kutekeleza agenda ya ukuaji wa viwanda na mageuzi ya uchumi, TBL imesisitiza kuwa itaendelea kuwekeza nchini, kushirikiana na jamii pamoja na kuunda thamani ya kudumu kupitia biashara inayozingatia uwajibikaji.